The Hill Youth TV Magazine..#guys,keep on moving.

Katika pitapita zangu kwenye mtandao nikakutana na hizi picha..honestly zimenigusa but sijui ni kwanini labda ni kwa sababu ni watu niliona nao karibu au kwa kuwa wapo na Diamond..sijui ni kwaini... nahisi ni mazingira ya SJMC -Mlimani TV ndo yamenishawishi zaidi.. but nnachoweza kusema.... kazi nzuri....keep on moving.
Herieth-host wa The Hill Youth tv Magazine akiwa na Diamond
Mitambo ikiwekwa sawa
Busy kwa kazi
Kazi imekamilika
Teacher Issa full tabasamu..naona dress code ilikua ni black n white
Noticeboard ileeeee!!


A guy fakes his death to make her Girlfriend see how Life would be Empty without Him


In what may very well be the worst wedding proposal in history, a Russian man hired a whole film crew to stage a deadly car crash and see if the woman he wanted to marry really loved him to death. 
Most people already know, or at least think they know the person they want to marry truly loves them, before they pop the big question, but 30-year-old Alexey Bykov, from Omsk, Russia, wanted to make absolutely sure. Instead of taking the easy route, like making his girlfriend Irina take a lie detector test, he decided to fake his own gruesome death to see what her reaction would be. So the young Russian hired a movie director, stuntmen, make-up artists, and even a script writer to stage a car crash in which he lost his life. They made sure everything looked as realistic as possible, by using crashed cars, smoke, ambulances and carnage, so the poor girl didn’t for a minute think she was the victim of a very creepy prank.

Once all the details of his plan were discussed with the film crew, Alexey arranged to meet Irina in a certain place, only when she arrived she found mangled cars and her beloved’s body lying on the road all covered in blood. A paramedic told her he was dead and she immediately broke into tears. Once the “romantic” prankster got the reaction he was waiting for, he got up from the pavement and proposed. You can imagine Irina’s reaction, can’t you? Well, although she admits at first she “almost killed him again, but for real this time”, in the end she accepted to be this crazy man’s wife for the rest of her life.
Asked why he planned such a macabre wedding proposal, Alexey Bykov said: ”I wanted her to realise how empty her life would be without me and how life would have no meaning without me.” Very romantic stuff, I must say. He did promise this was the last time he pulled such a stunt.
courtesy of odditycentral

Picha hii ya Dr Slaa na mtoto wa marehemu Daud Mwangosi yawaliza wengi..

Mtoto wa marehemu Daud Mwangosi akimkumbatia Katibu mkuu wa CHADEMA Dk Willbroad Slaa jana jioni wakati alipokwenda kutoa pole nyumbani kwa marehemu..Marehemu Mwangosi ameacha mke na watoto wannne.
Kila anaeiona picha hii anaguswa kwa namna yake..na  hizi ni baadhi ya comments zilizotolewa na wasomaji wa blog ya mjengwa.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema na aipe nguvu familia yake katika wakati huu mgumu

Safari ni safari

Vijana wa Kijiji cha Nkuhi Kata ya Isuna, Mkoa wa Singida, wakisafiri kwa baiskeli huku mmoja wao akiwa amelala katika mwamba, hali hilo inatokana na shida ya usafiri katika eneo hilo. (Picha na Prona Mumwi/MAJIRA)
Picha na wavuti.com

Wale ambao hamjahesabiwa sensa..toa taarifa kwa namba hizi...

-- Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imeongeza mbele tarehe za kumaliza kazi ya Sensa ya Watu na Makazi hadi Jumamosi ya tarehe 8 Septemba mwaka huu ili kuhakikisha kuwa kila mwananchi aliyebaki anahesabiwa. Hivyo wito umetolewa kwa mwananchi hawajafikiwa na Makarani wa Sensa watoe taarifa katika Ofisi za Serikali za Mitaa au Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa ajili ya kuhesabiwa. Kamishna wa Sensa kutoka NBS Hajjat Amina Mrisho ametoa  wito kwa wale ambao hawajaandikishwa hadi hivi sasa kuwa wanatakiwa watume taarifa kwa namba 2122724, 0754583415, 2129622 , 0713335429, 0713574622 na 0713312699

Na sisi tumevaa viatu

Wakiwa safi wamependeza na sare zao za shule..Kwa staili hii sidani kama hiyo elimu itakaa kichwani.

pic from mjengwablog

Picha hii imenikumbusha mbali...

Kiukweli hii picha imenikumbusha mengi..kipindi niko primary yaani timekeeper nae alikua na power kama kiongozi(kiranja) mwingine hivyo watu walikua wanaipigania hii nafasi.
Halikadhalika nikiwa secondary...yaani tulikua darasa moja na timekeeper  sio siri tulikua tunamshawishi agonge kengele kabla ya muda wa break ili wadau tukapige uji..!!Sipati picha na vyuoni kungekuwa na timekeeper?!!
Timekeeper kazini
Picha kwa hisani ya mjengwa

Waandaaji Wema VS Wolper lawamani!!


Katika kulizungumzia tamasha la Matumaini lililofanyika Uwanja wa Taifa Jumamosi iliyopita, moja ya vitu vilivyowavuta wengi ni pambano la ngumi kati ya Wema Sepetu na Jackline Wolper, kwa sababu ilikua ni kitu cha tofauti kutokea kwa hapa kwetu….kuwapambanisha wasanii maarufu ambao sio mabondia. Kwa hakika ilikua ni kitu kilichoongeza msisimko kabla ya tamasha kuanza kwa sababu kila mmoja alitaka kuona wadada hao wakitoana manundu.
Cha kusikitisha kinyume na matarajio ya wengi pambano lile halikua na mvuto kama ilivyotegewa, kwani hakuna ngumi zilizorushwa zaidi ya Wema na Wolper kurukaruka ulingoni, kuchekacheka na kushikanashikana kusipokua na sababu na mwishowe kuwachosha mashabiki na kuwafanya kutoa lawama zao katika vyombo vya habari na mtandaoni.
Hebu tujiulize  Wema na Wolper si waigizaji wa filamu??hivi walishindwa kabisa kuigiza kama wanapigana kweli??Hapana kwa hakika wanauwezo wa kufanya hivyo,ila uzembe na lawama zote zinaenda kwa waandaaji wa mpambano ule kwa kushindwa kujipanga na kukosa ubunifu…..
Ubunifu ulikosekana ilikua katika uandishi wa script (mwongozo) wa kusimamia pambano lile au kama script ilikuepo basi alieandika hakujua  nini cha kufanya…..kwani script yake ilishindwa kuwafanya Wema na Wolper wapigane kiuongo na kweli, iilshindwa hata kuwafanya warushe makonde na kuwatoa kijasho mfano ukiangalia vizuri ile sehemu Wema aliyokimbia na kwenda kumkumbatia refa ilikua ni nzuri lakini ya kijinga kwa sababu Wolper hakurusha ngumi ambayo ingemfanya Wema akimbie…hata kama walikua wanaogopa kuumizana basi script ilitakiwa iwaongoze sehemu za kupigana mfano mikononi n.k…...kwa kufika mbali zaidi script ingetakiwa hata itoe mshindi mmoja ili baadae hata waweze kuandaa pambano la marudiano ambalo lingewawezesha kupata fedha nyingi zaidi na kufanikisha ujenzi wa mabweni ya wasichana kama ilivodhamiriwa

Hakika tulichokiona ilikua ni kuchoshana kwa ufupi Wema na Wolper hawakupigna waandaji walitakiwa kuonesha pambano la  ukweli ….mfano mzuri  wrestling (mieleka) mapambano mengi yanaongozwa na script na  mshindi anapangwa lakini bado wapiganaji wanapigana kiukweli..hii ni kwa sababu lengo linakua ni kutoa burudani kwa watazamaji.

UDINI NA TANZANIA: TULIPOTOKA,TULIPO NA TUELEKEAPO


MCHANGO WA MOBHARE MATINYI KATIKA MJADALA WA UDINI

Naomba nichangie hapa kama Mtanzania - na si kama mwislamu au mkristo au mpagani.

1. Kwanza ni kweli kwamba kitabu cha yule padri mzungu kinaleta shida sana mawazoni mwa watu, Dkt. Sivalon. Lakini turejee kwenye ukweli wa kisomi, kwamba huwezi kuhitimisha jambo zito kwa kutumia chanzo kimoja. Hatuna maandiko mengine ya watu wasiokuwa na upande yanayothibitisha aliyosema bwana huyu. Hakuna utafiti wowote. Aidha, ni muhimu pia kuchunguza kujua alisema hivyo katika mazingira gani. Kuna Mkenya mmoja London aliwahi kuzuliwa na wenzake kwamba ni shoga na akatengwa kabisa. Aliyemzulia siku moja akamwambia Mkenya mwingine ninayemfahamu, kwamba anajua fika kuwa bwana yule si shoga lakini alifanya vile kumlipizia kisasi cha ugomvi wao. Uongo ulibadilishwa kuwa ukweli. Je, tuna hakika na maneno ya huyu mwandishi padri? Najua ukivutia upande mmoja itabidi useme uhakika upo kwa sababu kuna uthibitisho mwingine, lakini hali halisi inagoma. Nitaeleza.

2. Pili, ingawa Mwalimu Julius Nyerere analaumiwa sana na waislamu au watetezi wa waislamu, lakini kiukweli kama si yeye, hali ya kielimu ya waislamu nchini ingekuwa mbaya sana. Tusisahau kuwa, tulipopata uhuru serikali ya Mwingereza hakituachia shule za kutosha. Wakristo na dini za Waasia wakiwemo Wabohora, Waismailia na Wahindu walikuwa na shule lakini Waislamu hawakuwa na shule. Sasa ukumbuke pia kuwa, wakoloni wa Ulaya walikuja Afrika Mashariki kwenye karne ya 19 wakati wakoloni wa Uarabuni walikuwa tangu karne ya 13. Kwa miaka 600 Waarabu hawakujenga shule hata moja; bali walijenga madrasa kwa ajili ya masomo ya dini - jambo ambalo halikuwa dhambi. Shule za kwanza zilijengwa Tanganyika na Mjerumani zikiwa ni za darasa la kwanza hadi la nne kwa kutumia Kiswahili. Zanzibar zilijengwa sana sana na Mwingereza. Tafuta maana na historia ya maneno haya: (i) Darasa/Madarasa (ii) Shule (iii) Skuli. Kimsingi, Nyerere ndiye aliyezitaifisha shule za wasiokuwa waislamu ili na watoto wa waislamu waende kusoma kwa sababu walikuwa wanakwepa kubadilishwa dini na kulishwa nguruwe ingawa wakristo wengine kama wasabato hawali nguruwe.


3. Nchi yetu ikapiga hatua zaidi na tukaanza kujenga shule za msingi. Nyerere akajenga shule kwa juhudi kubwa zaidi kwenye mikoa iliyokuwa nyuma, ambayo mingi ilikuwa ni ya pwani waliko waislamu wengi zaidi. Haikutosha, baada ya Nyerere kuibana mikoa mingine, ambayo wananchi wake waliamua kujijengea wenyewe, akaweka nafasi maalum kwa watu wa makabila ambayo hayakuwa na watoto wengi shuleni, yaani hayakuwa yanataka shule. Waliofaidika zaidi ni makabila ya pwani ambako shule ilikuwa kama kituo cha polisi kwao. Dini yao wengi wao tunaijua. Mwalimu akiwa anaongoza TANU na CCM akajenga shule za jumuiya ya wazazi kwenye mikoa ya pwani na hata alipopata msaada kutoka Kuba (Cuba), aliichagua mikoa ya pwani pia kujengewa shule, na ndipo tukapata shule kama Kibiti, Ruvu, n.k. Hata ile ya Waswidi ilijengwa Kibaha. Alifanya hivi kuwasaidia hao mnaowaita waislamu (mimi nawaita Watanzania). Kule kwingine kama Kilimanjaro, wakaamua kujenga shule za binafsi zao wenyewe na ndio maana hadi leo wanazo nyingi. Serikali ya Nyerere haikujenga shule za sekondari kule bali ilijenga hizo chache kwenye mikoa yenye waislamu wengi. Ndio ukweli huo ila watu hawataki kuutafuta. Rekodi zipo, tafuta shule zote uone.

4. Serikali ya Tanzania haikuishia hapo. Wakati wa Rais Mwinyi waislamu wakiongozwa na Waziri Kighoma Malima walilalamika sana. Zikafanyika juhudi nyingi ikiwemo kumweka Malima kwenye sehemu kama elimu ambapo alianzisha awamu mbili za kwenda shule, lengo likiwa kuongeza idadi ya watoto wa kiislamu wanaoingia sekondari ingawa na wakristo pia waliongezeka. Pia Tanzania ikapata nafasi za masomo kwenye mataifa ya Misri, Algeria, Iran, na Uturuki, maalum kwa ajili ya waislamu tu. Marafiki zangu walikwenda huko na walinithibitishia kwamba hii ilikuwa maalum kwa waislamu tu. Bado waislamu waliendelea kwenda nchi zingine zisizokuwa za kiislamu bila tatizo. Huu ulikuwa msaada mkubwa.

5. Ikaja serikali ya Ben Mkapa na yenyewe ikaweka rekodi ya kuipa dini moja majengo ya chuo kikuu. Leo hii kipo chuo kikuu cha waislamu Morogoro kwa kutumia majengo ya serikali. Serikali ya JK imejenga shule nyingi sana za sekondari nchi nzima na sijasikia ubaguzi kwa upande wa mikoa yenye waislamu wengi. JK pia amehakikisha waislamu wanaongoza wizara ya elimu ili kuondoa malalamiko, na si kweli kwamba eti asiyekuwa mwislamu akiwa waziri wa elimu, basi waislamu wanashindwa kusoma. Hakuna ukweli hapa.

6. Najua kuna malalamiko mengi kuhusu shule na hata hospitali za misheni, lakini tuzitendee haki. Hizi ni za kuhudumia Watanzania wote, na ndiko Kikwete na binti yake waliposoma, hata Mzee Makamba. Tuweni wakweli kwenye hili. Waislamu wanatibiwa kote huku, na ruzuku ndiyo mkombozi wa Mtanzania mnyonge.

WAISLAMU KWENYE VYEO NA ELIMU

7. Labda, tuje kwenye hili moja: KWA NINI HATUNA WAISLAMU WENGI KATIKA NAFASI ZA JUU SERIKALINI? Hili jambo ni la kweli lakini inabidi tujiulize swali jingine zaidi: KWA NINI KUNA MADAI KWAMBA WAISLAMU HAWAJASOMA?

8. Nianze na historia yetu. Waarabu walipokuja kwenye karne ya 13 walileta vitu kadhaa vikuu vikiwa ni dini nzuri ya Kiislamu na pili utamaduni wao wa kishenzi. Ndiyo, walileta utamaduni wa kishenzi. Utamaduni wa Kiarabu siyo dini ya Kiislamu na dini ya Kiislamu siyo utamaduni wa Kiarabu. Uislamu ndio ulioongoza elimu duniani kwenye karne ya saba na nane na hata vyuo vikuu vya kwanza duniani vilikuwa vya Waislamu, lakini si Waislamu wote hupenda elimu, kama ilivyo kwa dini zote zingine pia. Ukienda kwenye nchi za Maghrebu na baadhi ya Mashariki ya Kati, yaani Moroko, Algeria, Tunisia, Misri na zile za Uturuki, Siria, Iraki na Yodani, kuna waislamu wengi wenye elimu. Hapa Marekani wanaheshimika, mathalani, wahandisi mahiri hutoka Uturuki, Pakistan na India kwenye majimbo yenye waislamu.

9. Hali ni tofauti kabisa kule Ghuba kwenye nchi za Saudia Arabia, Yemeni, Kuwaiti, Omani, Katari, Imarata na Bahraini. Ghuba watu hawataki shule. Hawa wa Ghuba ndio walioletea ushenzi wao huu Afrika Mashariki kuanzia kule Somalia hadi Msumbiji kaskazini - kote huku kuna watu wenye utamaduni wa Ghuba wa kukataa shule. Hili liko wazi. Kwa kuwa Waarabu wa Ghuba ndio walioleta pia Uislamu, basi watu hujumuisha kwa pamoja tatizo la kukosa elimu kwa sababu za kuiga utamaduni wa Ghuba na dini nzuri ya kiislamu ambayo inajali elimu sana. Saudia watu ni vilaza watupu kiasi kwamba kuna Wamisri milioni moja na zaidi wanaofanya kazi za kisomi. Kote huko Ghuba kasoro Yemeni na Omani (kwa sababu ya umaskini wao) kuna wageni wengi ndani ya nchi kuliko wenyeji kwa sababu watu hawataki shule.

10. Waislamu wa pwani ya Tanzania, kama wenzao wote wa Somalia yote, Lamu, Malindi, Mombasa, Zanzibar, Mafia, Kilwa, Lindi na Pemba ya Msumbiji, wana utamaduni wa Waarabu wa Ghuba wa kugomea shule. Tofauti na wenzao, waislamu wa Tanzania walioko Machame na Usangi mkoani Kilimanjaro, au Bukoba, na hata wale wa kabila la Waganda (Baganda) kule Uganda, wao wanapenda shule. Maeneo yote waliyokaa Waarabu, kuanzia Bagamoyo nenda hadi Tabora/Nzega, na Ujiji, shule si mali kitu. TATIZO SI UISLAMU BALI UARABU WA GHUBA. Anayebisha hongera zake.

11. Tafiti mbili ninazozijua, nitazisaka baadaye, zinasema kwamba kwenye miaka ya nyuma kama ya 1990, pale UDSM waislamu walikuwa ni kati ya 14 - 15% ya wanafunzi wa shahada ya kwanza wote. Hiki ni kiasi kidogo mno lakini ni kidogo cha kiasi gani? Lazima tujue hili nalo, hata kwa makadirio tu.

12. Nyerere aliamua tuachane na sensa ya kupekua dini za watu kwa sababu nzuri kabisa - alitaka Watanzania tusitambuane kwa dini zetu (na makabila pia). Hivyo, ili kuweka usawa tukaanzisha msemo huu: Tanzania sisi nusu ni Waislamu na nusu ni Wakristo. Huu ni msemo tu na hauna usahihi. Pili, hata kama sensa ya zamani ilionesha kwamba waislamu ama wakristo au wapagani ndio wengi, haina maana yoyote leo wakati taifa letu lina watu milioni 45 hivi. Tulipata uhuru tukiwa milioni 12 na baadaye Zanzibar ikaongeza laki tatu. Watanzania hatukuwa na kelele za asilimia ngapi ni dini hii na ile. Leo zimerudi.

13. Kwa mujibu wa taarifa za kitafiti (siyo mimi), Waislamu nchini Tanzania ni theluthi moja ya watu wote. Naomba Nasser na Salim muende mkamuulize rais wetu, Jakaya Kikwete, kwamba kwa nini alipoteua mawaziri mwaka Novemba 2010 aliweka theluthi moja waislamu, na kisha manaibu akafanya hivyo hivyo? Pia, muulizeni, kwa nini alipoteua mawaziri hii juzi, aliweka 1/3 waislamu na kwenye manaibu akafanya hivyo hivyo? Kabla hamjaenda, chukueni rekodi zenu kwanza muone. Jiulizeni pia, kwa nini wajumbe wa Tume ya Kupitia Katiba ya Muungano, wale wa Bara, theluthi moja tena ni waislamu? Rais Kikwete, nijuavyo mimi, anajaribu sana kuliangalia hili suala la kelele za dini ili asiharibu nchi yetu. Anakuwa mwangalifu sana, hata kama kuna wakati anateleza. Je, mahesabu yake haya yana maana gani? Nina hakika anajua anachokifanya na kamwe hawezi kuwaonea waislamu wenzake ambao ni Watanzania kama yeye. Hawezi kufanya uonevu.

14. Zifuatazo ni taarifa zinaonesha idadi ya waumini wa kiislamu nchini Tanzania:

(i) 35% = http://www.qran.org/a/a-world.htm.
(ii) 29 - 35% = http://en.wikipedia.org/wiki/List_of_countries_by_Muslim_population or The Future of the Global Muslim Population (Pew Research Center), http://pewforum.org/future-of-the-global muslim-population-preface.aspx
(iii) 35% = http://www.state.gov/j/drl/rls/irf/2010_5/168434.htm.

15. Hiyo taasisi ya kwanza ni ya kiislamu. Sijaweka za Wakristo kwa sababu sitafuti ushindani na siamini kama idadi ina maana yoyote, lakini kwa kuwa watu mnataka kupigia kelele, basi mzigo huo hapo. Mwaka jana mwanaharakati mmoja wa Tanga alikuja Marekani na akasema mkutanoni kwenye chuo kikuu kimoja kwamba waislamu ni 70% ya Watanzania wote, na pia kuna mwislamu mmoja mwenyeji wa Songea aliandika makala ya kitaaluma na akasema kwamba waislamu Tanzania ni 55% lakini akashindwa kueleza wanaishi wapi. Huyu wa 70% alishindwa pia kusema wanakaa wapi ambako hawaonekani. Pointi ni kwamba madai haya ni ya kijinga. Makala nyingine iliyoandikwa na msomi huyu Mtanzania ilisema kwamba Uganda wapo 45% na Kenya 33% na Msumbiji 40% (kama sijakosea). Hakuna popote duniani, hata kwenye mashirika ya kimataifa ya kiislamu zinapotajwa namba hizi za 55% kwa Tanzania na hao wengine wa Afrika Mashariki. Mashirika ya kiislamu yanasema kwamba Tanzania ina 30 - 35% tu. Ili kuleta amani, naomba tuseme kwamba Tanzania haina Wakristo kabisa, hata mmoja hayupo isipokuwa wale wenye madaraka serikalini. Tukumbuke pia, marais wetu wote watano wa sasa (kule Zenji na kwenye Muungano) ni waislamu.

16. Kwa nini idadi inakuwa muhimu hapa, achilia mbali kelele? Ni kwa sababu tunataka kuielewa ile 14-15% ya UDSM ambayo huenda hivi leo imeshabadilika kwa kuwa tuna vyuo vingi nchini. Tunahitaji maelezo, kwamba hao waislamu wengine wameishia wapi? Jibu lake linarudi kwenye ule UTAMADUNI WA WAARABU WA GHUBA. Hakuna mwislamu anayeonewa wala anayenyimwa shule. Mimi nimekulia na kusomea Dar es Salaam kwenye waislamu wa kutosha kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha sita, na JKT kabisa. Waislamu wote marafiki zangu waliokuwa wakali darasani waliendelea na elimu ya juu. Shule ya msingi tulikuwa watoto wanne machachari, mimi, Waziri, Salum na Izihaki, na wote tulifaulu. Vijana wa mwaka mmoja nyuma yetu pale Azania walikuwa na Mpemba aliyepata pointi SABA. Alikwenda tena Tambaza akawa nyuma yetu na akapata pointi TATU. Akaenda Ulaya. Hakunyimwa nafasi yoyote. Mwaka niliomaliza kidati cha sita kijana aliyeongoza Tanzania nzima alikuwa Karim, na yeye pia mwislamu. Hao wanaonyimwa wako wapi?

17. Kwa hiyo, kama 1/3 tu ndio waislamu (walau kinadharia), na pia wengi wao wako pwani kwenye utamaduni wa Ghuba usiotaka shule, tunashangaa nini wakienda wachache vyuo vikuu, tuseme 20%? Je, watakuwaje sawa serikalini na Wakristo ambao walianza utamaduni wa elimu tangu enzi hizo? Ni suala la historia tu lakini si kwamba ukiwa mwislamu huwezi kwenda shule.

OMBI

Tufanye juhudi kuwakomboa wale wote walio nyuma kielimu Tanzania. Wako wengi, kwa dini na makabila, lakini wote ni Watanzania. Walio nyuma wasiseme kuna uonevu, bali waondoe kilichowakwamisha. Hatuwezi kulinganisha utamaduni wa elimu wa watu wa Kilwa, Mafia, Rufiji na Pangani, na watu wa Moshi, Kyela, au mkoani Kagera. Tuwe wakweli. Mwenyezi Mungu hapendi waongo. Kwa nini shule za binafsi hazina pia waislamu wengi? Nani anawazuia waislamu kujenga shule Tanzania? Je, kama kweli unataka mtoto wako apate elimu safi, na amekosa nafasi ya shule ya serikali, utampeleka wapi? Pale Kinondoni Muslim? Tuseme ukweli.

Naamini tunao uwezo wa kuyatatua matatizo yetu ya kihistoria na kitamaduni na si kukaa chini kupanga vurugu kwa madai ya kuonewa. Waislamu wa Saudi Arabia hawajasoma licha ya utajiri wao. Je, hao nao waziri wao wa elimu na baraza la mitihani ni ya Tanzania? Kwani waislamu wa Uturuki, Tunisia, Misri, Senegal na Afrika Magharibi yote wana elimu?

Tutafute chanzo cha kweli cha tatizo, halafu wote tushirikiane kulitatua; wote kabisa.

AOTA MATITI BAADA YA KUTUMIA ARV's


Mkaazi wa kijiji cha Magomeni Wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani,  Khamisi Tanga (46), ameota  matiti katika hali isiyo ya kawaida ikidaiwa imesababishwa na kutumia dawa za kupunguza  makali ya Ukimwi   ARV’S.  

 Akizungumza na waandishi wa habari waliokwenda Wilayani humo kufanya utafiti kuhusu utekelezaji wa sheria ya Ukimwi na Chama cha Waandishi wa habari za Ukimwi (AJAT),Khamisi (Pichani) alisema alipatwa na mkasa huo miaka mitatu iliyopita.    Akisimulia namna alivyoanza kuugua alisema awali aliona matiti yake yakiongezeka ukubwa kila kukicha lakini hakujua kama lingeweza kuja kuwa tatizo kubwa kama lilivyo sasa.    Baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya ilimbidi kwenda kliniki anayohudhuriaga kupata dawa na kuwaeleza manesi ambapo walimjibu kuwa imesababishwa na dawa anazotumia na hivyo kulazimika kukatizwa dozi hiyo na kupewa aina nyingine.
   
Hata hivyo Khamisi alisema kwamba pamoja na kubadilishiwa dozi hajaona kama kuna mabadiliko yoyote aliyoyapata na kuongeza kwamba hivi karibuni alipewa dawa nyingine ambazo kati ya hizo kuna zile ambazo zilimsabishia matiti na tayari ameanza kupatwa na maumivu aliyokuwa akisikiaga awali wakati matiti yalivyokuwa yanaanza kuota.

Kwa mujibu wa Khamisi ameshahangaika kupata matibabu hadi Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili lakini hadi leo hajapatiwa tiba stahili ya kumaliza tatizo hilo.    “Jamani Watanzania naomba wanisaidie kwa njia yoyote ile ili niondekane na hali hii kwani inanidhoofisha sana na kunikosesha raha hasa mbele ya wanaume wenzangu."Kwani hapa navyoongea na nyie waandishi nilipimwa hadi kansa na matiti ndio kama hivyo mnavyoyaona yanaendelea kukua na huniuma sana hasa wakati ninapolala,”alisema Khamisi  

Pia ametumia fursa hiyo kumuomba Rais Jakaya Kikwete kumsaidia ili arudi katika hali yake ya uanaume kwa kuwa maisha kwa sasa kwake yamezidi kuwa magumu kwa kuwa hawezi kufanya kazi yoyote kutokana na hali hiyo.

Mtaalam wa magonjwa, Dk. Dina Komakoma,akielezea kuhusu sababu za kutokewa kwa hali hiyo kwa wagonjwa wenye maambukizi ya VVU ni jambo la kawaida japo hutofautiana.Dk. Komakoma alisema wengine hujikuta wakinenepa au wakikonda sana na hili la Khamis sio mtu wa kwanza kupatwa na hali hiyo na kuongeza kwamba inapotokea mgonjwa akapata hali tofauti kama hiyo anapaswa kusitishiwa dawa.

 kwa hisani ya MICHUZI



   

Agonising death of the King of the Jungle:


It is a heartrending sight.
Wire snare caught so tightly around his neck he cannot eat, this young male lion is doomed to die a slow and agonizing death. Within a matter of days he will be lying in the African bush gasping his last breath.
 
Nor is he alone in his grim fate. The sight is increasingly common in parts of the continent when a growing number of lions have fallen victim to poaching. Some wander by mistake into snares that are meant for other animals such as antelope which are hunted by poachers for bush meat.
 The young male lion cub was spotted in Mikumi National Park with a poacher's snare twisted cruelly round his neck

Others, whoever, are being deliberately poached for their body parts.
There is now a growing demand for lion claws and bones in parts of the Far East for use in traditional medicines. The huge animals are hunted more and more as a substitute for tigers, whose body parts have traditionally been used for the Chinese medicine market.
Tigers are now so scarce in the wild that poachers have turned to another target.
A sharp increase in the lion bone trade suggests that these are being swapped for tiger bones. Pelts and claws are also being used.
Doomed to die: The wire was twisted so tight that the lion was unable to eat
Dr Pieter Kat, from LionAid, said: 'There has been a huge jump recently in the value of lion bones driven by the traditional medicine market, seeing as we have so few tigers.
'Since tiger bones are now so difficult to obtain there has been a switch to lion bones.'
In the 1990s, 1kg of lion bones was worth just $10, but now that has massively increased to $300 in 2010.  And its reflected in the figures that show the populations of lions are on a serious decline. There were an estimated 200,000 lions in Africa in the sixties. This has dropped massively now to just 23,000- 25,000.
The final journey: The lion slopes off into the long grass of the park where he would soon die either of starvation or infection
A source said: 'Only a few weeks ago we saw this lion with a snare around its neck in Mikumi National Park in Tanzania. 'The park rangers tried to track it with the intention of trying to remove the snare from around its neck, but by the time they arrived at the location, the lion had disappeared into the bush. It wouldn’t have survived for many more days. Already the wound was gaping, open to infection and covered in flies.
'And it was so tight around its neck that it would have found it impossible to eat. It would have either died from infection or starvation.'

WANAHABARI WETU:: KEEP ON DREAMING!!!


                                                                                                                             pic kwa hisani ya wavuti

Homa matokeo kidato cha 6...sintofahamu yazidi kwa watoto wa wakulima


Zikiwa zimebakia siku chache kwa matokeo ya kidato cha sita 2012 kutoka, homa”   juu ya hatima ya vijana waliofanya mtihani huo imezidi kuongezeka. Joto hili limezidi kuongezea sio tu kwa kuhofia ufaulu wa mtihani yao bali kilichoongeza sintofahamu ya  hatma yao kwenda vyuoni, wengi wahofia kushindwa kumudu gharama za elimu ya juu kwani hali ya kupata ufadhili kutoka bodi ya mikopo (HESLB) umeanza kuonekana  kuwa mgumu (tete).

Kukata tamaa huku kumechangiwa zaidi na taarifa zilizotolewa na TCU kupitia kitabu cha mwongozo wa udahili 2012/2013-Admission guide book 2012/2013. Katika kitabu hicho ambacho licha ya kutoa vigezo vinavyohitajika ili mwanafunzi achaguliwe kwenda kusoma katika chuo husika pia wametoa mchanganuo wa utoaji wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2012/2013. Katika mchanganuo huo  unaonyesha vipengele viwili ambavyo ni Possible Loan amount na Loan Priority. Katika kipengele cha loan priority kinaonyesha kozi (taaluma) ambazo zimepewa kipaumbele cha kupewa mkopo, hivyo kupelekea kuwepo kwa makundi mawili ambayo ni Priority na Non Priority. Kwa ufupi non priority ni wale ambao hawana uwezekano wa kupata mkopo. Hivyo possible loan amount kinawahusu wale ambao ni priority (watakopata mkopo)

Cha kusikitisha zaidi, ni kwamba asilimia 96 ya kozi zote zinazotolewa na vyuo mbalimbali ni non priority isipokuwa kwa wataochagua Education, Engineering na Medicine,Kilimo na kozi nyingine baadhi za sayansi. Hiki ni kizungumkuti kwa wale waliokuwa na matumaini ya kusoma Biashara, Uchumi, Political Science, Sheria, Uandishi wa Habari, na kozi nyingine zilizobaki kwani upatikanaji wa mikopo kwao ni ndoto. Sijui ndugu zangu watoto wa wakulima waliosoma EGM, HGE, HKL, HGL, HGK KLF nk watakimbilia wapi? Kimbilio liliobaki ni education pekee, tena watakaomudu kusoma hii  ni wale waliotoka kwenye familia zenye auheni kidogo (middle class) kwani bodi wanatoa ufadhili wa 50% kwa watakaosoma education;  lakini kwa mtoto wa mkulima choka mbaya kupata elimu ya chuo asahau.

Wazee wa IFM  mpo??chuoni kwenu hakuna kozi hata moja inayokula mkopo??
Uwezo wa kumudu gharama za ada, (tuition fee), chakula na malazi (meals & accommodation), na fedha nyingine za kujikimu zitapatikana wapi? Gharama hizi mzigo usiobebeka na wazazi wengi hawawezi kumudu gharama hizi. Hiki ni kilio, tena kisicho na mfiwa maalumu..wafiwa ni watoto wa masikini ambao ni tuko wengi hapa Tanzania. Kwa hali hii watakaosoma vyuo ni watoto wa matajiri tu! watoto wa wakulima twende wapi?  kwenye mabenki tukachukue mikopo ya kujisomesha? Inasikitisha kuangalia kitabu hicho cha TCU. 
Hii ni chinja chinja mpaka wazee wa Mzumbe panga hili limewapitia
Nashindwa kuelewa nini maana ya mkopo?hivi fedha hizi si hurudishwa pindi mwombaji anapomaliza masomo? Au ndo serikali haina fedha kama tunavyosikia? Huku ni kutowatendea haki watoto wa masikini walio na kiu ya kupata elimu ya juu. Tena ni uonevo mkubwa..njooni vyuoni mtazame maisha ya wanafunzi wa mwaka jana waliokosa mkopo..maarufu kama NO LOAN…nadhani kupitia hili umuhimu wa kuwapatia wanafunzi mikopo unaweza kuonekana. 
Sio kwenu tu IFM ndo hakuna mkopo?vyuo kibao kama CBE,Ustawi, Tumaini,KIU,bodi hawatoi mkopo pia



Matokeo hayo ya kidato cha sita yanatarajiwa kutoka mwisho mwa mwezi huu kama ilivyo ada. 
Wazee wa SUA

HILL mpo??



Itazame hii halafu unipe maelezo!!

Hebu iangalie na wewe hii picha kwa sababu nimeshindwa kuitolea maelezo..(caption)!!Pia sifahamu kilichokuwa kinawaliza hawa  watoto..jaribu ku-share na sisi kilichopo kichwani mwako.

Bi Joyce Banda rais mpya Malawi.

Aliyekua makamu wa rais wa nchini Malawi,Bi Joyce Banda ameapishwa kuwa rais wa nchi hiyo.Hii imekuja kufuatia kifo cha raisi Bingu wa Mutharika.  Banda anakuwa rais wa kwanza wa kike kusini mwa Jangwa la Sahara, na amepishwa mbele ya bunge katika mji mkuu wa Lilongwe Malawi.
Bi Joyce Banda rais wa kwanza mwanamke kusini mwa jangwa la sahara

Bi Banda, ambaye alikuwa makamu wa rais tangu mwaka 2009, alishangiliwa na kupigiwa kofi kabla na baada ya shughuli hiyo. Bw Mutharika, 78, alipatwa na mshtuko wa moyo siku ya Alhamis, ingawa kifo chake hakikuthibitishwa hadi Jumamosi. Kuchelewa kutangazwa kifo chake kulisababisha wasiwasi kuhusu nani anaongoza nchi hiyo. Kulikuwa na tetesi kuwa watu wa karibu wa rais Mutharika walikuwa wakitaka kubadili katiba ya nchi ili kuzuia Bi Banda kuchukua madaraka, na badala yake kumpa ndugu yake, Peter Mutharika ambaye ni waziri wa mambo ya nje. Bi Banda alifarakana na rais Mutharika mwaka 2010 na kuwa mkosoaji mkubwa wa rais. Alifukuzwa kutoka chama cha DPP na kuunda chama chake cha Peoples Party

Kauli ya Hussein Bashe kuhusu ushindi wa Arumeru


Kwanza nitumie nafasi hii binafsi kuwapongeza CHADEMA kwa ushindi wa Arumeru Mashariki, Kiwira, Kirumba, Liziboni na Pia CUF kwa ushindi wa Kata ya Tanga

Nimeamua kufanya hivi kwa misingi ya kidemokrasia ni wapongeze mmepewa heshima hiyo watumikieni.

Nawapongeza pia kwakua uchaguzi huu kama viongozi wa CHAMA changu watatumia Busara basi hili ni funzo kubwa, na nina washukuru CDM (chadema) matokeo haya kutupa ishara kuwa Kaskazini inaanza kupotea mikononi mwetu, Kusini Nyanda za Juu inaanza kupotea, Kanda ya Ziwa inaanza kupotea hii ni Alarm kwa CHAMA change, umewadia wakati kwa ujumbe huu viongozi wakuu warudi katika Round Table kujadili upya na kutazama kama makundi yetu yatakisaidia CHAMA


Kwa matokeo haya Kanda ya ziwa alikuwepo Samwel Sitta ,kwa maana ya Kirumba, Mbeya alikuwepo Mama Anne Kilango, kwa Maana ya Kiwira, Arumeru alikuwepo Mzee MKAPA, Mzee Mkama, Mzee Lowasa, Ndg yangu Nape, Liziboni Dk Nchimbi na maaneo haya yote, Tumeshindwa umewadia wakati wa KUJITAFAKARI na kujiangalia kwa kina na si kuja na majibu kama yale tuliokuja nayo Baada ya Uchaguzi Mkuu 2010, Tunatakiwa kuja na MAJAWABU.

Nadhani demokrasia imeheshimika na CCM tumekua tukisahau wajibu wetu wa kujadili matatizo ya watu toka mwaka 2007 Mpaka sasa 2012 , wananchi walitupa 1st Workup call 2010 hatukuamka and this is a 2nd Workup Call hatuna Budi kuwashukuru wananchi bcs Wametupa 2nd chance ya kuamka Tujitafakari UPYA

Nimelizie kuwwapongeza CUF na CDM kwa Ushindi wao niwatakie kila la kheri Asanteni kwa kutuamsha mara ya pili.

kwa hisani wavuti