HATUWEZI KUENDELEA KWA NCHI ILIYOJAA WANYOA VIDUKU!!

  Nafurahishwa sana kwa kuona muamko mkubwa wa Watanzania wengi  kutaka kuwa na maendeleo katika nchi yetu, hamasa hii inatokana  na kufunguka kifikra na kiakili miongoni mwa watu hivyo kupelekea kujitambua na kujua haki zao na kipi wa wanachokitaka  kiwepo katika jamii yetu. Lakini kwa masikitiko makubwa napenda kuwa vunja moyo kwa kuwaambia kuwa HATUWEZI kupata maendeleo kwa taifa lililojaa wanyoa viduku na wavaa supra!!” .   Najua unajiuliza kwani kuvaa supra na konyoa kiduku  kuna mahusiano gani na suala la maendeleo?? Sina  maana ya wazi kiiivo ,naamanisha kuwa suala la maendeleo hushangiwa kwa kiasi  kikubwa na kupevuka kwa fikra kwani hata Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa” Umasikini wa fikra ni umasikini mkali kuliko yote” lakini wengi wetu hasa vijana bado hatujataka  kuzipevua akili zetu bali tumezidi kuzidumaza fikra zetu kwa kufikiria kunyoa viduku,kuvaa  kata K, huku tuikimba Muhogo andazi, Muhogo andazi, na kwa sauti kubwa tunaimba ni sababu ya Ulofa na nyimbo nyingine za mahadhi hayo. Zaidi ya hapo tunafikiria ni lini tutaenda kupiga picha za editing kule my fair au photo point! Kubali kataa hayo ndio mawazo ya sisi vijana wa leo. Mfano mzuri ni wengi wa wanamuziki wetu vijana hawatoi nyimbo zenye hamasa kwetu.