Kauli ya Hussein Bashe kuhusu ushindi wa Arumeru


Kwanza nitumie nafasi hii binafsi kuwapongeza CHADEMA kwa ushindi wa Arumeru Mashariki, Kiwira, Kirumba, Liziboni na Pia CUF kwa ushindi wa Kata ya Tanga

Nimeamua kufanya hivi kwa misingi ya kidemokrasia ni wapongeze mmepewa heshima hiyo watumikieni.

Nawapongeza pia kwakua uchaguzi huu kama viongozi wa CHAMA changu watatumia Busara basi hili ni funzo kubwa, na nina washukuru CDM (chadema) matokeo haya kutupa ishara kuwa Kaskazini inaanza kupotea mikononi mwetu, Kusini Nyanda za Juu inaanza kupotea, Kanda ya Ziwa inaanza kupotea hii ni Alarm kwa CHAMA change, umewadia wakati kwa ujumbe huu viongozi wakuu warudi katika Round Table kujadili upya na kutazama kama makundi yetu yatakisaidia CHAMA


Kwa matokeo haya Kanda ya ziwa alikuwepo Samwel Sitta ,kwa maana ya Kirumba, Mbeya alikuwepo Mama Anne Kilango, kwa Maana ya Kiwira, Arumeru alikuwepo Mzee MKAPA, Mzee Mkama, Mzee Lowasa, Ndg yangu Nape, Liziboni Dk Nchimbi na maaneo haya yote, Tumeshindwa umewadia wakati wa KUJITAFAKARI na kujiangalia kwa kina na si kuja na majibu kama yale tuliokuja nayo Baada ya Uchaguzi Mkuu 2010, Tunatakiwa kuja na MAJAWABU.

Nadhani demokrasia imeheshimika na CCM tumekua tukisahau wajibu wetu wa kujadili matatizo ya watu toka mwaka 2007 Mpaka sasa 2012 , wananchi walitupa 1st Workup call 2010 hatukuamka and this is a 2nd Workup Call hatuna Budi kuwashukuru wananchi bcs Wametupa 2nd chance ya kuamka Tujitafakari UPYA

Nimelizie kuwwapongeza CUF na CDM kwa Ushindi wao niwatakie kila la kheri Asanteni kwa kutuamsha mara ya pili.

kwa hisani wavuti