Tamko la BAVICHA kuhusu wanafunzi waliofukuzwa vyuoni.

       Kwa miaka ya hivi karibuni Vyuo mbalimbali vimekua na tabia yakuwafukuza ama kuwasimamisha masomo wanafunzi wanaoendelea na masomo kwenye vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini mwetu kutokana na mashinikizombalimbali kutoka kwa viongozi wa kiserikali kwa kisingizio kuwa wanafunzi hawa wanafanya siasa vyuoni.Itakumbukuwa kuwa migomo na maandamano ya wanafunzi kwa vyuo vikuuhapa nchini haijaanza pale mfumo wa vyama vingi uliporuhusiwa kuanzamwaka 1992 ,bali migomo na maandamano haya yamekuwepo tangu kuanzishwa kwa vyuo hivyo.Mathalani, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimekuwa na historia ya migomo na maandamano ya mara kwa mara tangu kuanzishwa kwake , na hivyo dhanaya kuwa wanafunzi wanagoma kutokana na misukumo ya kisiasa sio sahihihata kidogo bali ni mbinu ya watawala kujaribu kuficha madhaifu yao .Wanafunzi hawa wamekuwa wakigoma kutokana na serikali ya CCM kuendeshamambo yake kibabe na kwa dharahu ya hali ya juu ambapo imefanya elimukuwa Privilage na si haki kwa watanzania.

Kwa mantiki hiyo basi, kutokutendewa haki kwa wanafunzi hawa naserikali yao, kukosekana kwa miundombinu bora ya kusoma na kujifunzia,wanafunzi hawa kunyanyaswa na watawala wa vyuo hivyo, kukosekana kwamikopo kwa wakati muafaka, serikali kuingilia uendeshaji wa vyuo ,serikali kuvunja serikali za wanafunzi bila kutoa sababu za kimsingi na sababu nyingine mbalimbali ndio chanzo cha vurugu na migomo vyuoni.

Hivyo basi , kutokana na sababu tajwa hapo juu Baraza la Vijana na CHADEMA (BAVICHA) tunatamka wazi kuwa kitendo cha Vyuo Vikuu vya Dar Es Salaam, Dodoma na Muhimbili kuwafukuza wanafunzi kwa ujumla wakez aidi ya 100 ni kitendo cha uonevu kwa wanafunzi hawa na kamwe hakivumiliki hata kidogo na haswa ikizingatiwa kuwa ni watoto wa watu masikini na ambao kimsingi wanajilipia ada wenyewe kwani wanakopa na baada ya muda watapaswa kulipa fedha hizo.
Kwa nini tunapinga uamuzi huu wa kuwafukuza wanafunzi vyuoni;
 
1. Ni kinyume na Tamko la Ulimwengu la mwaka 1990 la uhuru wa kitaaluma (Academic Freedom) ambalo tulisaini mnamo mwezi April tarehe29 hapa Dar Es Salaam , linasema wazi kuwa ni lazima Vyuo vijiendeshe kwa uhuru kamili bila kuingiliwa na serikali .
2. Kufukuzwa kwa wanafunzi hawa ni utekelezaji wa Maazimio ya vikaovya CCM vilivyofanyika na haswa vile vya Halimashauri Kuu ambavyo vimetoa maelekezo mbalimbali kwa Serikali juu ya kuwachukulia hatua wanafunzi wa vyuo vikuu ambao wamekuwa wakiikosoa serikali waziwazi ,na hata wahadhiri ambao wamekuwa wakitumia taaluma zao kwa uwazi nakusema juu ya mapungufu ya serikali wachukuliwe hatua ya ama kufukuzwa kazi  au ajira zao kusitishwa. Hivyo hii ni muendelezo wautekelezaji wa maamuzi hayo. 


Nothing to stop you,just do it!!


 Nimesimama tayari kwa kuanza kufanya, lakini sijui nianzie wapi? Sio kama sijui  ninachotaka kukifanya, HAPANA!!nakifahamu fika ,tena akili  imelipangilia jambo hilo vizuri, tatizo macho yanaona lakini  hayaoni mwanzo wake!! Mikono na miguu ina nguvu lakini vimepatwa na kigugumzi haviwezi kufanya lolote!!  Chakusikitisha  domo langu gundi linashindwa kusema, ili nisaidiwe kuoneshwa mwanzo eti kisa nafsi inaogopa kuchekwa!  

   Hofu imezidi kuingia nafsini,  tena nazidi kuogopeshwa kwa lugha ya kizungu eti “time will tell” kwa tasfiri rahisi wanamaana eti nisubiri mpaka muda utakapozungumza! tangu lini muda ukawa na mdomo ?! tena sijui unazungumza lugha gani? Ghalfa nawakumbuka wahenga, wanananiambia “ngoja ngoja ya huumiza matumbo!” nami naingiwa na hofu ya kuumwa tumbo. Akili inazidi kufunguka na kuuona kuwa wakati ni ukuta, hivyo hakuna wakati mwingine wa kuyafanya haya. Muda ndo huu, akilini inakemea hofu, nguvu ya uthubutu inajaa nafsini, mara napokea muujiza, macho yanaona mwanzo mpya, mikono na miguu viko tayari kufanya kazi! Gundi lililojaa mdomoni linayeyuka ghalfa napata kusema, wengine wanadharau na kuona kile ninachotaka kufanya hakina maana, Sivunjiki moyo! wapo wanaonipa moyo nakuona uzuri wa kile ninachotaka  kufanya. Nainza safari ya kufanya, nilikuwa sioni mwanzo lakini sasa nauona. Safari inaendelea tena kwa mwendo wa LORUUU KEIKEI….sijali vikwazo vya njiani mpaka nitakapofika kwani siku zote “the end justify the means” kwani mwisho ndio utakaonipa majibu ya hiki ninachokifanya.

  Wengi tunateswa na ugonjwa huu,ni gonjwa la HOFU inasemekana wengi tunaugua ugojwa huu! mambo yetu mengi hayaendi kisa hofu, wengine stress (msongo wa mawazo) zinazidi kisa hofu. Dawa imegundulika kuwa ni kujipa moyo, uthubutu na kujiamini. Kataa hofu na if you want to do, DO IT NOW hakuna wakati mwingine.