Kila ufikiriapo ndipo mafanikio yako huongezeka!!!


Tukumbuke ndugu zangu,mawazo ndiyo mwanzo wa mafanikio yako. Unapokuwa na ndoto mafanikio kwanza yakupasa kuwa na wazo ambalo baadae utalifanyia kazi, ili utengeneze bahati yako. Kwa kufuata maelekezo hayo utakuza upeo wa fikra zako.

Wengi wanaweza wasikutendee haki, kama wengi wafanyavyo, wanaweza kukupotosha katika uhuru ulionao, lakini hawawezi kukuchukulia mawazo unayoyawaza. Kutokana na fikra zako utakuwa unashinda siku zote. 

Unataka kuwa na furaha? Unataka kuwa na amani? Unataka kuwa na cheo, nguvu au utajiri? Fikiri kuwa navyo, utafanikiwa. Fikra unazowaza ni muhimu kuliko ujuzi ulionao. 
Ujuzi una mipaka, mawazo yanatawala muda wote, yanaleta maendeleo. Kila mtu binafsi anakuwa na ndoto za mafanikio bila kujitambua. Kwa mfano, wazazi wanapopanga ni jinsi gani watawaendeleza watoto wao, wajasiriamali wanapopanga ni jinsi gani wataendeleza biashara zao hiyo yote ni mifano ya kuwa na ndoto njema ya mafanikio. Watu wachache wamejifunza kutumia mawazo yao kwa faida lakini wengi wetu mawazo tuliyonayo yanapata kutu kutokana na kutoyafanyia kazi. Hakuna sababu ya kuona aibu katika dunia ya ubunifu.

Kuwa na mawazo ya kufanya jambo fulani ni kitu kizuri katika dunia hii tunayoishi. Kila mmoja wetu ana kiwanda chake cha kuwa na mawazo. Lakini ni wapi mawazo hayo yanapotoka? Ni wapi waandishi, wana sayansi na wabunifu wanapopata mawazo makubwa? Kwa nini baadhi ya watu wengine wanakuwa wabunifu zaidi ya wengine? Ni kutokana na kutumia vizuri mawazo yao.

 Kila mmoja wetu, kwa wakati mmoja au mwingine, lazima kujifunza chanzo halisi cha mawazo. Utajiri, unaweza kuupata, inategemeana na ulivyoyaweka mawazo yako. Wazo dogo rahisi linaweza likabadilisha kabisa maisha yako uliyonayo.  Pia huwezi ukajua ukubwa wa mafanikio yako mpaka utakapojifunza jinsi ya kuchanganya juhudi zako na mawazo yako.  Kwa vyovyote unapotaka mafanikio unajitathmini wewe mwenyewe. Mwili uliopumzika una nguvu, vile vile akili. Kama unataka kuwa mbunifu na mpokeaji wa mawazo mapya, inakubidi kupata muda kwa mawazo hayo na kuyafanyia kazi.
Jizoeze kila siku kuwa na muda wa mapumziko, chagua chumba kizuri kilichotulia au kiti kizuri ambacho kitakusaidia kutuliza akili kwa urahisi. Unavyoendelea kujifunza kupumzika, utapata mawazo ambayo yatakufikisha katika malengo na matarajio yako.

Mtunzi anafikiri juu ya uimbaji, mchoraji anafikiri juu ya rangi, mwandishi anafikiri juu ya habari na maneno. Kama utachukua wazo moja na kulitendea kazi litakupa matokeo mazuri. Yafanyie kazi mawazo yanayokujia. Kuwa na utayari katika kunasa mawazo yako. Mawazo mengi mazuri yanapotea kwa sababu hayawekwi katika maandishi.

Tathimini mawazo yako. Mara tu unapomaliza kuyachuja mawazo yako, unachagua yale unayotaka kuyafanyia kazi. Utagundua kuwa nayo yanahitaji kuongezewa ubora wake. Jifunze ndugu yangu kutokufunga milango yako ya kuwa mbunifu.


Makala hii imetoka kwa Seif Kabele

UDPRSA 5th anniversary marked a new beginning!!

Celebration of the 5th anniversary of University of Dar es Salaam Public Relations Student Association (UDPRSA) has marked an opening way in which all UDPRSA members and other PR professional s in the industry to communicate and interact easily on matter concerning their career, this is due to the launching of their blog and face book page.

   While speaking to members the guest of honor and the main speaker his excellence Professor Eno Akipabio encourages leaders and members to be committed and insists leaders to come up with new ideas that will strengthen their association. He further said through such association will enable them to exchange their ideas, creating networks professionals and utilize the opportunities that face them as students. Prof Akipabio went on saying the opening of blog and facebook page is great achievement especially at this era of development of social and new media.
The display which shows UDPRSA blog
However, on his remarks Mr Amin Antony Mgeni who was among the founders of UDPRSA said he is happy to see the association still exists and he advise leaders to take quick solution to whatever challenge encounter the association. Mr Mgeni who is currently an editor at Mlimani tv, encourages members to use the blog in writing articles and feature stories hence would enable them to become good PR’s. 
On the left is Mr Kisoma Mussa and Mr Amini Mgheni one of the founder of UDPRSA
“This 5th anniversary is a challenge to me and my cabinet, we ensure that UDPRSA will still move on, but without your cooperation (members), UDPRSA won’t succeed” said the new President of UDPRSA, Mr Kisoma Mussa. He added that up to this time they succeed to create a network with association like University of Dar es Salaam Markerting Association (DUMA), Saut Student Public Relations Association (SSPRA) and currently they are in discussion with Public Relations Association of Tanzania to see on how they can work together.

From the left is UDPRSA vice president Mr Raymond,Bonnie-UDPRSA deputy GSProf  Akipabio and Kijanga
The 5th anniversary celebration was held on 10th November at School Journalism and Mass Communication and was attended by the Director of Publicity at DUMA, Mr Enock Ngulwa, media people and other alumni of SJMC.
UDPRSA members during 5th anniversary event.

HATUWEZI KUENDELEA KWA NCHI ILIYOJAA WANYOA VIDUKU!!

  Nafurahishwa sana kwa kuona muamko mkubwa wa Watanzania wengi  kutaka kuwa na maendeleo katika nchi yetu, hamasa hii inatokana  na kufunguka kifikra na kiakili miongoni mwa watu hivyo kupelekea kujitambua na kujua haki zao na kipi wa wanachokitaka  kiwepo katika jamii yetu. Lakini kwa masikitiko makubwa napenda kuwa vunja moyo kwa kuwaambia kuwa HATUWEZI kupata maendeleo kwa taifa lililojaa wanyoa viduku na wavaa supra!!” .   Najua unajiuliza kwani kuvaa supra na konyoa kiduku  kuna mahusiano gani na suala la maendeleo?? Sina  maana ya wazi kiiivo ,naamanisha kuwa suala la maendeleo hushangiwa kwa kiasi  kikubwa na kupevuka kwa fikra kwani hata Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa” Umasikini wa fikra ni umasikini mkali kuliko yote” lakini wengi wetu hasa vijana bado hatujataka  kuzipevua akili zetu bali tumezidi kuzidumaza fikra zetu kwa kufikiria kunyoa viduku,kuvaa  kata K, huku tuikimba Muhogo andazi, Muhogo andazi, na kwa sauti kubwa tunaimba ni sababu ya Ulofa na nyimbo nyingine za mahadhi hayo. Zaidi ya hapo tunafikiria ni lini tutaenda kupiga picha za editing kule my fair au photo point! Kubali kataa hayo ndio mawazo ya sisi vijana wa leo. Mfano mzuri ni wengi wa wanamuziki wetu vijana hawatoi nyimbo zenye hamasa kwetu.