HII NDIYO AFRIKA YETU.

    Naamini bara la Afrika ni moja ya sehemu iliyobarikiwa sio tu kwa rasilimali zilizopo bali pia kuwa na watu wenye nguvu kuliko sehemu nyingine duniani. Lakini cha ajabu ndio sehemu inayoongoza  kwa matatizo kama vita (vurugu),ufukara,ufisadi,njaa na ukame kuliko sehemu  yoyote.Sijui tatizo letu ni nini??. Wapo wanaosema eti WAAFRIKA TUMELAANIWA!! Mimi siamini kwamba tumelaaniwa kwani Mungu hawezi kuwa katili na muonevu kwa Waafrika kiasi hicho,tatizo lipo sehemu limejificha,kuzungumzia LAANA ni uvivu wa kufikiri  na uwoga wa kuumiza kichwa katika ufumbuzi wa matatizo yanayotukabili.


    Kwa upande mwingine inaniingia akilini kwamba yaweza kuwa laana,tena iliyotoka kwa shetani, hii inatokana na matendo yatunayofanya waafrika. Mfano mzuri ni hali inayoendelea huko pembezoni mwa afrika katika nchi ya Somalia,kwa muda wa miezi mine sasa imekumbwa na ukame na njaa illiyosabisha njaa kali kwa wananchi na mifugo yao. Hali hii imesababisha vifo vya mamia ya watu hasa watoto na wengine maelfu kukimbilia nchi za Kenya na Ethiopia kama wakimbizi.

Baadhi ya wakazi wa Somalia waliokimbilia Kenya
   
 Kutokana na hali hii mashirika ya kibinadamu kama Save the children wamekuwa wakitoa huduma mbalimbali kwa wakimbizi kwa wananchi wa Somalia na wamekuwa wakitoa taarifa kuwa hali inazidi kuwa mbaya kadiri siku zinavyosonga mbele. Cha kusikitisha zaidi ni kwamba wafanyakazi wa shirika hili wamekuwa wakivamiwa na waasi hivyo kukwamisha zoezi la utoaji wa misaada. Hata baada ya umoja wa maataifa kupitia shirika la kuhudumia wakimbizi UNHCR na mradi wa chakula duniani (World Food Programe) kuamua kwenda kutoa  misaada ya chakula,waasi hawa wa Alshabab wameanzisha mapigano makali dhidi ya mashirika haya,huko mjini Mogadishu.

Mama wakisomali akiwa na mwanae
   Hakika huu ni ukatili wa hali ya juu,licha ya kuona wenzao(ndugu zao) wanasulubika kwa tatizo la njaa bado wameamua kuwazuia kupata chakula hicho. Nahisi lengo lao ni kuwamaliza kabisa.Kwanini waafrika tumekosa utu na huruma kwa wenzetu? Kwa hali hii zoezi la kuwanusuru ndugu zetu wasomali na baa hili la njaa limeingia dosari,hivyo tuzidi kuomba miujiza ili Alshabab wasitishe mapigano na watoto,vijana na wazee wa Somalia wanusurike na njaa inayowakabili.
  

HAVE YOU THOUGHT THIS??

Hapa kwetu Tanzania tumezoea kusikia  mtu akiwa chuo basi anasoma sheria, udaktari, engineering, uhasibu, Human Resources( HR) au Ualimu lakini hii tofauti kwa wenzetu kwani  hutumia  gharama kubwa kusomea fani nyngine mfano mapishi..

I thought making ice-cream was pretty easy, but it seems that if you really want to get it right you have to take courses at the Gelato University, in Bologna, Italy.

Lango la kuingilia chuoni hapo.
  Ice-cream making was one of the last thing I would have imagined required attending a university, but in reality thousands of students from all over the world study the art of making quality ice-cream at the Carpigiani Gelato University, in Bologna, every year. Gelato lovers, and entrepreneurs who want to learn the secrets of making great ice-cream and take it back to their homelands pay around €800 ($1,138) for a week of courses and accommodation at a nearby hotel. They attend technical lectures on traditional gelato-making techniques by veteran ice-cream makers, and take part in practical courses where they learn to use the world famous Carpigiani gelato machines.

Hapa ni baada ya Presentation yao.

Believe it or not, the Carpigiani Gelato University has been around for a long time, and as more people around the globe fall in love with the Italian gelato, it gets more students with each passing year. In 2011, the number of students has gone from 9,000 to 12,000 and for the first time in history, the number of foreign tourists has surpassed that of Italians.
  
Washikaji wakiwa katika lecture  fromhttp://odditycentral.com

HII INA KUHUSU MTUMIAJI WA INTERNET!!

  Katika dunia ya sasa suala mifumo ya upokeaji wa taarifa  na mawasiliano (information and communication technology-ICT) kwa sasa limekua sana, sio tu kwa nchi zilizoendelea hata kwa nchi zinazoendelea mfano mzuri ni hapa nyumbani Tanzania,tumeona kwa kiasi chake maendeleo ya mifumo ya digitali na satelaiti( digital & satelite),na intanet vikiongezeka kwa kasi.Chakusikitisha ni kwamba badala ya maendeleo haya kutusaidia kusonga mbele,sasa yamegeuka kikwazo cha sisi kufikia maendeleo yanayohitajika kwa mfano uwepo wa intaneti sio  tu kwa kutuvunjia maadili bali hata kwa kutupotezea muda mwingi wa kufanya shughuli nyingi za kimaendeleo.Kwani hivi sasa watu hutumia muda mwingi ku-chat kwenye facebook au twitter.Kibaya zaidi kinachozungumzwa humo ndani ni upuuzi usiojenga.

Jamaa kakomaa na surakitabu       (pic wavuti.com)
    Kwa wenzetu vitu vinawasaidia sana sio tu katika mawasiliano bali hata kutangaza biashara zao,katika elimu (online education) na zaidi hata kutoa nafasi za ajira.Tofauti kabisa na hapa kwetu,bado tuna ile kasumba ya kizamani ya kuhisi kuwa facebook ipo kwa ajili ku-upload picha tu.Unaweza kukuta mtu amekesha internet lakini anachokifanya hakina manufaa.Imefika wakati tubadilishe mitazamo yetu,tutumie vyombo hivi kwa namna itakayotuletea manufaa.

THIS IS TOO MUCH!!

    Tafiti nyingi zilizokwishafanyika zinaonyesha kuwa kwa kiasi kikubwa nyani na wanyama wengine jamii ya sokwe wanafanana na binadamu sio tu kwa sura(muonekano),mfumo wa uzazi halikadhalika matendo yao kwani mambo yote anayofanya binadamu nao nyani wanauwezo wa kufanya vizuri.  
Hapa ameshika bunduki aina ya AK 47! (www.wavuti.com)
Hapa sijui anafikiria familia yake??!!

   Wataalam wanasema tofauti iliyopo kwamba binadamu ana uwezo mkubwa(IQ) wa kutambua mambo kuliko nyani.Pia tendo aliloweza nyani ni kuzungumza(produce sound speech).


VITA HII UDSM MPAKA LINI??

  Hali  ya ulinzi na usalama katika mazingira ya chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) imezidi kuwa mbaya kutokana na kuongezeka kwa vitendo vya wizi na ukabaji.Mara hii imefikia pabaya zaidi kwani wezi wamekuwa wakitumia silaha kama mapanga na visu kufanyia uhalifu huo na tumekuwa tukishuhudia wenzetu wakijeruhiwa vibaya na kuporwa mali zao kama laptop,fedha au simu.Cha kusikitisha uhalifu huo umefikia kwenye hatua ya ubakaji kwani tumesikia dada yetu mmoja amepatwa na mkasa huo hivi karibuni.Tunawapa pole wote waliopatwa na maswahibu hayo.Tujiulize hawa wanausalama wetu (auxiliary police) wako wapi wakati haya yanatokea?Vipi management  ya chuo inafahamu haya?wamejipanga vipi kutuhakikishia usalama wetu?

Huu ndio ulikuwa mwanzo wa safari ya kifo cha kijana huyo ambae hakujulikana  jina.
 Kwali hali hii,hatua za makusudi inabidi zichukuliwe haraka,kwani cha kutisha wamekuwa wanaingia kwenye hostel (hall of residence) bila woga.Ni hivi karibuni tu Hall 5 na Hall 2 wamekamata na kuwapa kipigo wezi hao kisha kuchukuliwa na Auxiliary Police,lakini hatujui hatma yao.Labda hatua za kisheria zinaendelea?!!Kama ndivyo,basi inabidi zifanyike haraka na umma kupewa taarifa kwani maafa yaliomkuta mwizi wa juzi yametokea kutokana na kuona sheria hazitekelezwi hivyo wanafunzi wakaamua kuchukua sheria mkononi.Lakini tujiulize kumuua mwizi ni suluhisho la tatizo hili?

    Japokuwa inauma sana kuona wenzetu wanapata ulemavu, kupoteza mali za thamani  na  muda wa masomo kutokana na uhalifu waliofanyiwa na wezi hawa,lakini kitendo cha kumpiga na kumtesa mtu hadi kufa ni kitendo cha kinyama kisicho na utu hasa kwa wasomi wa chuo kikuu.Hata maandiko yameandika “alipizae ubaya kwa ubaya huyo ni shetani”, “isitoshe akupigae shavu la kulia mgeuzie la kushoto’.Hata katika sheria za uislamu (Islamic Sharia) adhabu ya mwizi imesemwa ni kukatwa mkono na sio kifo!kwanini tusingeamua hata kufuata sheria hii labda ingeweza kuwa funzo? Thamani ya uhai wa mtu hailinganishwi na kitu chochote.

    Tutafakari kwanini yule binti wa Kizungu alipiga kelele “stop it,stop it, it’s against human rights” nahisi hakuwahi kuona katika maisha yake unyama kama ule, pia hakuwahi kudhani mwanadamu wenye akili timamu anaweza kufanya vile.Japo tulimdhihaki kwa kumwambia “eti Human rights unazijua leo,wakati mnawatesa babu zetu enzi za slave trade hamkuziona??”tukamtimua eneo la tukio!!hapo ndipo tulipodhihirisha udogo wetu wa kufikiri na kwamba elimu tunayoipata haijatukomboa.Inabidi tukubali kwamba its completely against humanity. Yatupasa kutubu kwa Mungu na dhambi ile isitutafune.

Binti wa kizungu aliyejaribu kutetea uhai wa kijana yule.
   Tujiulize tumefanya vile kwanini?ni kulipiza kisasi au  ni kwa kujipoza kwa maswahibu yalowakuta wenzetu au ni kutoa funzo kwa wezi wengine??Hofu yangu ni kwamba wezi hawa wakiamua kuungana na kulipiza kisasi kwa mauaji yaliompata mwenzao na uhakika tutakuwa katika hali ya hatari zaidi!!Wao wana uwezo zaidi,wakiamua kutuwinda kwa mishale au kuja kutuchomea moto tukiwa hosteli??! MUNGU AEPUSHE MBALI BALAA HIZI!! Kweli usalama wetu ni mdogo na hatari ipo kwetu zaidi. Vita hiyo hatutoiweza.Tunahitaji sheria madhubuti ambazo zitatoa adhabu kali na kuwa fundisho kwa wahalifu,kwani imeonekana kuwa ongezeko la kuchukua sheria mkononi ni kutokana wananchi kuchukizwa na hali ya wahalifu kuachiliwa huru bila kupewa adhabu yoyote.Na imani kwa sala ya mwisho aliyoombewa na dada yetu kabla ya kukata roho, marehemu mwizi atapumzika kwa amani.

Akiwa tayari amekata roho!!