Che Mundugwao arudi na Kandindi





Baada ya kukaa kimya kwa miaka miwili, mwanamuziki wa miondoko ya Asili, Che Mundugwao a.k.a Mtoto wa Lulindi ametoa nyimbo yake mpya inayoitwa KANDINDI. Akizungumza na modreamz, Che Mundu amesema KANDINDI, inazungumzia maisha yake halisi ya wakati akirudi nyumbani kwao Lulindi Masasi na  mchanganyiko wa ladha ya asili na ladha ya mziki wa sasa (Bongo Beats). Ameongeza kuwa nyimbo hiyo ameimba kwa lugha ya Kiyao kwani hata jina lenye lina maana ya ndege aitwae Mdiria au King fisher kwa Kiingereza. Halikadhalika Che Mundu amesema nyimbo hiyo itakata kiu ya mashabiki wake waliokua wakimsubiri kwa muda mrefu.