WALIOTOKELEZEA SJMC PUBLIC LECTURE


Mzee Charles Irigo akiendesha mhadhara

Associate Dean SJMC Dr Andililile

Wadau walikuwepo

Dr Ayoub Chacha Rioba akifuatijia mahadhara kwa makini

Mzee Samwilu Mwafisi akiendesha majadiliano

Saed Kubenea, kwa nyuma ni mama Eda Sanga

Mwl Dominic Makukula akichangia mada.

Wadau wakifuatilia mhadhara
Tajiri Malela

Aggie a.k.a Mama Alvin akifuatilia mhadhara

Maywili katika pozi

OGO busy na simu

I really like this Photo


Prof Thompson kutoka US alikuepo

Yasin a.k.a Kipacha shughuli kama hizi hukosekani

Cholo Boy akifuatilia mhadhara
Picha imetokaje?!

Kama sio SJMC vile

Kaka Khatibu nae alikuwepo kwa nyuma yake ni Peter Farayo

Hilali Ruhundwa kifanya mahojiano na Dr Rioba
Man at Work
Said Kubenea akisalimia na Dr Makoye Dean of SJMC

Dr Ayoub Rioba(kushoto), Deon of SJMC, Dr Herbert Makoye (katikati) na Said Kubenea(kulia) wakisalimiana baada ya PUBLIC LECTURE

SJMC PUBLIC LECTURE YAFANA

Na Hilali Ruhundwa


Vyombo vya habari hapa nchini vimetakiwa kufanya kazi kwa weledi wa hali ya juu kwa kutambua nafasi na mchango wake katika kukuza demokrasia licha ya changamoto zilizopo.  Hayo yamebainishwa na wataalam na wasomi waliobobea katika taaluma ya uandishi wa habari wakati wa mjadala kuhusu ushiriki wa vyombo vya habari katika kutatua migogoro na kuimarisha amani (the role of media in conflict resolution) pamoja na nafasi ya vyombo hivyo katika demokrasia ya vyama vingi (Media Accountability in Tanzania’s Multiparty Democracy) ulioandaliwa na hule uu ya uandishi wa habari na mawasiliano kwa umma (School of Journalism and Mass Communication) SJMC

Madam Zuhura Seleman
Katika mhadhara huo watoa mada walikuwa ni Dr. Ayoub Rioba aliyewasilisha mada kuhusu ushiriki wa vyombo vya habari katika demokrasia ya vyama vingi Tanzania (Media Accountability in Tanzania’s Multiparty Democracy) na Bi. Zuhura Sulemani akitoa mada kuhusu nafasi ya vyombo vya habari katika kutatua migogoro (The role of media in conflict resolution).

Akiwasilisha mada Bi Zuhura Selemain amesema kwa kiasi kikubwa vyombo vya habari vimekua kichocheo cha migogoro mbalimbali ya kisiasa, kidini na kikabila barani Afrika akitoa mfano wa mgogoro baada ya Uchanguzi(2007) nchini Kenya na mgogoro wa Burundi na Rwanda. Akihitimsha mada yake Bi. Zuhura amesema vyombo vya habari sio chanzo cha migogoro bali ni kichocheo cha migogoro iliyopo.


Dr Ayoub Rioba
 Kwa upande wake Dr Rioba amesema serikali inawajibu wa kutambua na kuthamini mchango wa vyombo vya habari kwani vinauwezo mkubwa wa kuitunza au kuharibu amani iliyopo Tanzania.
Mhadhara huo ulihudhuriwa na wadau mbalimbali katika sekta ya habari na  mawasiliano nchini akiwamo Bw. Samwilu Mwafisi aliyekua Mkurugenzi wa TUT( Taasisi ya Utangazaji Tanzania) kwa sasa ni TB, Mama Eda Sanga ambaye ni Meneja Uzalishaji,Mlimani Media Said Kubenea na Bw Mbwilo Kitujme Mhariri wa Habari TBC.