You are beautiful in your color!!

Nikiwa katika mihangaiko ya kazi nikaenda kwenye ofisi moja maeneo ya Ubungo. Nilipokelewa na mama mmoja (mlinzi) wakati ananipa utaratibu nilikuwa na mshangaa kwa masikitiko kwa jinsi alivyoharibika uso wake (kaungua na kuweka ukungu mweusi). Kwa nyakati hizi imekuwa kawaida kukutana na watu wa aina hii wengine utawakuta ni weupe kupitiliza, wengine wekundu, wengine wamebabuka yaani balaa tupu! sio tu akina dada bali hata akina kaka nao wamejiingiza katika matumizi ya Creams.
Moja ya wanawake walioharibika kutokana na matumizi ya vipodozi pic by modernghana

      Creams ninazozitahaja hapa ni lightening (bleaching) creams ambazo zime-contain mercury and hydroquinone, alpha hydroxyl acids, Arsenic,na nyinginezo nyingi.Kutokana na utafiti wa Dr S Allen Counter 2003 ilionekana kuwa sumu ya mercury (zebaki) imekutwa kwenye miili ya watu wengi wao wakiwa wanawake. Nchi zilizooneka kuwa vinara katika hili ni Mexico,Saudi Arabia, Senegal,Tanzania na nchi nyingine za Afrika magharibi. Sababu kubwa unayowafanya watu kuji-cream (kujichubua) ni kwa ajili kwa kutaka kuonekana warembo. Lakini hii ni kasumba mbaya kwani kuwa mrembo au kuonekana unapendeza ni lazima uwe mweupe? HAPANA tena tafiti zinaonyesha kuwa most beautiful and attractive women in the world are actually black women! Angalia akina Naomi Campbell, Halle Berry, Tyra Banks,Miriam Odemba, Nancy Sumari na wengine wengi. Kibaya zaidi tunaambiwa “Beauty is more than skin deep” . Athari kubwa zimekuwa zikionekana sana huku kwetu Afrika kwa sababu vipodozi hivi vingi haviko favorable na mazingira yetu kwani watngenezaji wanashauri watumiaji wasiwe wanakaa jua au watumie sunblock masharti haya wengi wa akina dada zetu yamewashinda!! Hivyo kujikuta wanababuka ngozi zao,  athari nyingine ambazo zinazowatokea ni kuzeeka kwa ngozi kutokana na mikunjo hivyo kumfanya kijana anaonekane mzee, kupata cancer hali kadhalika kifo chaweza kutokea kwa wale wanaofanya  plastic surgery.
Nancy Sumari one of the black beautiful girl
  Licha ya vipodozi hivi kupigwa marufuku katika nchi mbalimbali lakin bado vimekuwa vikiuzwa  kinyemela.Imeshauriwa kuwa watumiaji waepuke vipodozi vyenye chemical hizo au watumie vipodozi vya asili (HERBAL) ambavyo vinaweza kulinda urembo wao.
Jikubali ulivyo because you are beautiful in your natural color.

VOTE FOR Mt KILIMANJARO


   Ukiwa kama mdau wa unahimizwa kuuwezesha mlima Kilimanjaro kushinda na kuwa moja ya maajabu ya dunia. Hii ni kupitia shindano la new 7 world wonders linaloendeshwa hivi sasa. Mlima Kilimanjaro una mita 5895 kutoka usawa wa bahari  (5895 from the sea level)  una vigezo vyote vya kuingia katika  new world wonders, kwanza   kabisa ni mlima mrefu kuliko yote barani Africa, pia una vilele viwili ambavyo ni Kibo na Mawenzi zaidi ni kwamba, inastaajabisha kwa mlima kama huu (Volcanic mountain)  kuweko katika ukanda wenye hali ya hewa ya Kitropiki.
 Kuupigia kura ni rahisi tembelea www.new7wonders.com au bofya  hapahttp://www.new7wonders.com/vote-2?lang=en
      Lets unite & enable mount Kilimanjaro to be the new world wonder.