Mtazamo wa Kipanya kuhusu Mchakato wa Katiba Mpya# tuwachore tu


Mkasa mwingine wa Kusikitisha St. John University



Mwanafunzi wa uuguzi katika chuo Kikuu cha St. John kilichopo mkoani Dodoma na ambaye alikuwa muuguzi katika hospitali ya Kilimatinde, Manyoni, Singida amefariki dunia baada ya kubakwa na kisha kuuawa na watu wasiojulikana.

Mwili wa marehemu huyo aliyetambuliwa kwa majina Lyidia Mzima mwenye umri wa miaka 57, ulikutwa umetupwa kichakani na tayari ulishaliwa na fisi.



Inataarifiwa kwua marehemu alipatwa na masaibu hayo alipokuwa ametoka kujisomea, akiwa anarudi anakoishi katika nyumba ya kupanga, Kibaoni-Image B, katika kata ya Kikuyu Kusini, iliyopo karibu na chuo hicho.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, David Misime amethibitisha kutokea kwa tukio hilo juzi usiku na kwamba marehemu alionekana kunyofolewa nyama za mapajani.

Kiongozi wa wanafunzi wa chuo hicho aliongeza kuwa aliuona mwili wa marehemu ukiwa umechunika ngozi kuanzia utosini hadi sehemu ya kisogoni.

Mwili wa marehemu uligunduliwa na wananchi ambao walisema kwa siku mbili ilikuwa ikisikika milio ya sauti za fisi kutoka katika eneo ambapo mwili wa marehemu ulikutwa.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya rufaa Dodoma ukisubiri kufanyiwa uchunguzi.

Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Gabriel Mwaluko alithibitisha tukio hilo na kusema hayo yote yanatokana na chuo kukosa mabweni ya wanafunzi kulala jambo ambalo linafanya wanafunzi wengi kwenda kupanga mitaani na kukumbwa na matukio mbalimbali.

Mei mwaka jana, wanafunzi wa chuo hicho waligoma kuingia madarasani hadi wawasilishe malalamiko yao kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa, kutokana na kukithiri kwa vitendo vya kupigwa nondo, kuibiwa vitu kulawitiwa na hata kubakwa. Walisema sababu nyingine inayochochea matukio hayo ni chuo kukosa uzio na hivyo kurahisisha mwingiliano wa watu na wanachuo.

Hivi karibuni wanachuo wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Dar es Salaam waliandamana wakipinga kukithiri kwa vitendo vya wizi, ubakaji na ulawiti katika hosteli zao zilizoko Kigamboni.
source wavuti

MKASA MZIMA WA IFM #poleni sana

Huyu alishikiliwa mapema mara baada ya mabomu kuanza kupigwa, huku akionja joto ya jiwe ya askari hao ambao walionekana kuwa na uchu wakupiga.

Picha hii inakuonesha kwa karibu namna rungu lilivyompasua Askari huyu, hapa utapata fikiria kama huyu askari aliyepigwa kidogo tu baadaye akaachiwa ameumia hivi, Je! Wale waliopata mkong'oto wapo kwenye hali gani?


Baada ya kupata nafuu anakuja kumalizia hasira zake kwa wanafunzi kwa kumkamata mmoja na kumpa kipigo cha nguvu hadi askari wenzake walivyopiga kelele ndipo alimwachilia mwanafunzi huyo


Kundi la wanafunzi walishikwa kama kuku wa mdondo baada ya kupigwa mabomu ya machozi na kujikuta wakijificha sehemu moja kundi zima hali iliyosabisha kutembezwa kichurachura hadi kwenye kituo cha Polisi cha Kigamboni.


Mwanafunzi huyu alilala kabisa na kupoteza fahamu baada ya kuzidiwa na moshi wa mabomu ya machozi yaliyopigwa kwenye eneo la kituo hicho cha Polisi



Hakuishia hapo aliwafuata pale walipoamrishwa kukaa akawa anamchomoa anaemtaka na kumpa kipigo vile alivyojiskia ili amalizie hasira zake.

Askari huyo aliendelea kutoa dozi

                                   ANGALIA PICHA HIZI TATU KWA MAKINI


Alianza kwa kupandishwa kwenye gari

Ghafla alidondoka kwenye gari la polisi baada ya gari hilo kujaza wanafunzi wengi

Gar liliondoka yeye akaachwa chini

    Sijui kama dada huyo alisalimika kweli?
picha kwa hisani wavuti.com