Ulimwengu Jr & Princess washinda Mr & Miss UDSM 2011!!

Shindano la kuwatafuta Mr & Miss UDSM lilofanyika jana katika ukumbi wa Nkurumah,limemalizika kwa Jenerali Ulimwengu Jr kuchukua taji la Mr UDSM 2011 na kwa Miss UDSM mshindi ni Princess Chiaro.Washindi wengine ni Herieth Shija ambaye ni mshindi wa pili na na Anifa Issa ni watatu kwa upande wa mamiss.Mr UDSM na mbili ni Victor Hongoa na watatu ni Richius Kashonda.Katika mchuano huo mambo yalikuwa mazuri kwa upande wa Herieth Shija na Ulimwengu Junior kwani waliweza kunyakua tuzo za Miss & Mr Talents.Mshiriki mwingine aliyedhaniwa kuibuka kidedea ni Raheem Mkadara a.k.a Da Prince lakini upepo ulikuwa vibaya kwa upande wake na kuambulia kuingia Top five tu.!
Washindi wa Miss UDSM 2011 katika pozi la pamoja.Kushoto ni Herieth Shija mshindi wa 2,kulia ni Anifa Issa (3) na katikati ni Miss UDSM

Mr UDSM, Jenerali Ulimwengu Jr katika vazi la ubunifu.


Miss UDSM  2011 akivikwa taji.


Mr UDSM wakati wa kujibu maswali.
Kwa habari na matukio yaliojiri siku hiyo  bofya Photo Album page hapo juu.Picha na Hilal Ruhundwa