BINADAMU LAKINI MWILI SUMAKU!!

Ile hali ya kuwepo kwa binadamu walio tofauti na wengine inaendelea kuongezeka,kwani  huko  Croatia kaskazini mtoto wa miaka 6 aitwae Ivan Stoiljikovic ambaye amekuwa na hali ya kunasa vitu vya chuma (usumaku) katika kiwiliwili chake.Mtoto huyo ambaye pia kimwili umbile lake halilingani na umri,hilo halimpi halimzuii  kuvua chati na kuwaonyesha watu uwezo wake huo wa ajabu.
   Babu aitwae Ivan Surlovic anasema,alinza kuonesha maajabu tokea akiwa mdogo kwani  alianza kutembea akiwa na umri wa miezi nane,na kabla ya kufikisha miaka miwili alikuwa na uwezo wa kuendesha baiskeli,kitu ambacho kiliwashangaza.Babu yake anaendelea kusema, hali hiyo ya usumaku waligundua miezi michache iliyopita,wakati walipokuwa wakiangalia kipindi cha televisheni kilichokuwa kinamuonyesha kijana mwingine mwenye uwezo kama huo,nae Ivan ajijaribu kama utani, ghafla wakaona vitu vya chuma vinanasa pia kwake.
Familia yake inasema,hali hiyo huwa na nguvu zaidi nyakati za asubuhi akiwa ametulia,pia vyuma vizito hunanasa vizuri zaidi ya vile vyepesi.


Nzito lakini hapa ndo imenasa.

"Jamani ona mikono yangu ipo nyuma,sijaichika"

MUANGALIE HUYU JAMAA!!

Jamaaa mmoja ambaye hakufahamika jina lake,alifumwa akifuta viatu vyake kwa kutumia ulimi wake wakati akisubiri usafiri wa treni huko jijini New York.
Hizi ni picha za mshikaji akiwa katika harakati za kusafisha kiatu chake.

Check hii video yake uone vituko zaidi.

WEWE UNGEWEZA HII?


Check jamaa anavyomjali Ngamia wake!!hapa alikuwa anamfanyia medical checkup ya meno(pedicure).Daah sijui kama ingekuwa ni hapa nyumbani TZ kuna mtu angethubutu kufanya hivo?!
Kwa kawaida hapa Tanzania imezoeleka kwa wanyama hawathaminiwi ipasavyo.Kwa mfano pindi wanapoumwa maradhi au kupata tatizo la kuvunjika huwa wanaachwa bila msaada wowote.Kama ni mnyama anaelika basi huwa tunakimbilia kumchinja.

Huyu mwingine kaamua kumpeleka bata wake hospitali!!ingekuwa Kwetu bongo, KISU kingekuwa kinamuhusu bata na siyo hospitali!

Ulimwengu Jr & Princess washinda Mr & Miss UDSM 2011!!

Shindano la kuwatafuta Mr & Miss UDSM lilofanyika jana katika ukumbi wa Nkurumah,limemalizika kwa Jenerali Ulimwengu Jr kuchukua taji la Mr UDSM 2011 na kwa Miss UDSM mshindi ni Princess Chiaro.Washindi wengine ni Herieth Shija ambaye ni mshindi wa pili na na Anifa Issa ni watatu kwa upande wa mamiss.Mr UDSM na mbili ni Victor Hongoa na watatu ni Richius Kashonda.Katika mchuano huo mambo yalikuwa mazuri kwa upande wa Herieth Shija na Ulimwengu Junior kwani waliweza kunyakua tuzo za Miss & Mr Talents.Mshiriki mwingine aliyedhaniwa kuibuka kidedea ni Raheem Mkadara a.k.a Da Prince lakini upepo ulikuwa vibaya kwa upande wake na kuambulia kuingia Top five tu.!
Washindi wa Miss UDSM 2011 katika pozi la pamoja.Kushoto ni Herieth Shija mshindi wa 2,kulia ni Anifa Issa (3) na katikati ni Miss UDSM

Mr UDSM, Jenerali Ulimwengu Jr katika vazi la ubunifu.


Miss UDSM  2011 akivikwa taji.


Mr UDSM wakati wa kujibu maswali.
Kwa habari na matukio yaliojiri siku hiyo  bofya Photo Album page hapo juu.Picha na Hilal Ruhundwa 

TIBA JINGINE JAMANI!!

     Azerbaijan  ni moja ya nchi zinaongoza kwa uzalishaji na uuzaji mafuta dunia. Katika mji wake mkuu Baku, kumetokea hospitali inayojulikana kwa jina la Naftalan ambayo kwa miaka mingi sasa imekuwa ikitumia mafuta ghafi kama tiba ya magonjwa  mbalimbali ya ngozi  na mengine ya viungo na mifupa kama arthititis na rheumatism .  Katika tiba hiyo mgonjwa hutakiwa kujiloweka katika sinki lenye gallon 35 za mafuta hayo na kukaa ndani yake kwa muda usiozidi dakika kumi.Wagonjwa wengi wamesema hujisikia vizur wakati wapo ndani ya mafuta hayo hivyo kutamani  kukaa zaidi ya dakika hizo zinazopendekezwa na daktari. Meneja mkuu katika hospitali hiyo, Dr Alif Zulfugar amesema kuwa mgonjwa hatakiwi kuzidisha dakika pia haruhusiwi kutumia tiba hiyo zaidi ya mara moja kwa siku kwani inaweza kumletea madhara ambayo hakuyataja.Ameongeza kwa kusema tiba hiyo inatolewa kwa muda wa siku 10 tu.

Baadhi ya wagonjwa wakioga dawa hiyo




Jamaa akifutwa mafuta hayo baada ya kujiloweka


OSAMA AUWAWA.

 Rais Barrack Obama amethibitisha taarifa za kifo cha Osama Bin Laden,kiongozi wa kundi la Al-Qaeda ambaye ameuliwa katika operesheneni iliyofanywa na majeshi ya Marekani jana jumapili huko Pakistan katika mji wa Abbottabad.Kufutia taarifa hizo Obama amehaidi kuimarisha ulinzi katika Balozi zao kwani ana wasiwasi wa kutokea mashambulizi.
Osama enzi za uhai wake akiwa na viongozi wengine wa Al- Qaeda

Wamarekani wakishangilia taarifa za kifo cha Osama.