Tamko la BAVICHA kuhusu wanafunzi waliofukuzwa vyuoni.

       Kwa miaka ya hivi karibuni Vyuo mbalimbali vimekua na tabia yakuwafukuza ama kuwasimamisha masomo wanafunzi wanaoendelea na masomo kwenye vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini mwetu kutokana na mashinikizombalimbali kutoka kwa viongozi wa kiserikali kwa kisingizio kuwa wanafunzi hawa wanafanya siasa vyuoni.Itakumbukuwa kuwa migomo na maandamano ya wanafunzi kwa vyuo vikuuhapa nchini haijaanza pale mfumo wa vyama vingi uliporuhusiwa kuanzamwaka 1992 ,bali migomo na maandamano haya yamekuwepo tangu kuanzishwa kwa vyuo hivyo.Mathalani, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimekuwa na historia ya migomo na maandamano ya mara kwa mara tangu kuanzishwa kwake , na hivyo dhanaya kuwa wanafunzi wanagoma kutokana na misukumo ya kisiasa sio sahihihata kidogo bali ni mbinu ya watawala kujaribu kuficha madhaifu yao .Wanafunzi hawa wamekuwa wakigoma kutokana na serikali ya CCM kuendeshamambo yake kibabe na kwa dharahu ya hali ya juu ambapo imefanya elimukuwa Privilage na si haki kwa watanzania.

Kwa mantiki hiyo basi, kutokutendewa haki kwa wanafunzi hawa naserikali yao, kukosekana kwa miundombinu bora ya kusoma na kujifunzia,wanafunzi hawa kunyanyaswa na watawala wa vyuo hivyo, kukosekana kwamikopo kwa wakati muafaka, serikali kuingilia uendeshaji wa vyuo ,serikali kuvunja serikali za wanafunzi bila kutoa sababu za kimsingi na sababu nyingine mbalimbali ndio chanzo cha vurugu na migomo vyuoni.

Hivyo basi , kutokana na sababu tajwa hapo juu Baraza la Vijana na CHADEMA (BAVICHA) tunatamka wazi kuwa kitendo cha Vyuo Vikuu vya Dar Es Salaam, Dodoma na Muhimbili kuwafukuza wanafunzi kwa ujumla wakez aidi ya 100 ni kitendo cha uonevu kwa wanafunzi hawa na kamwe hakivumiliki hata kidogo na haswa ikizingatiwa kuwa ni watoto wa watu masikini na ambao kimsingi wanajilipia ada wenyewe kwani wanakopa na baada ya muda watapaswa kulipa fedha hizo.
Kwa nini tunapinga uamuzi huu wa kuwafukuza wanafunzi vyuoni;
 
1. Ni kinyume na Tamko la Ulimwengu la mwaka 1990 la uhuru wa kitaaluma (Academic Freedom) ambalo tulisaini mnamo mwezi April tarehe29 hapa Dar Es Salaam , linasema wazi kuwa ni lazima Vyuo vijiendeshe kwa uhuru kamili bila kuingiliwa na serikali .
2. Kufukuzwa kwa wanafunzi hawa ni utekelezaji wa Maazimio ya vikaovya CCM vilivyofanyika na haswa vile vya Halimashauri Kuu ambavyo vimetoa maelekezo mbalimbali kwa Serikali juu ya kuwachukulia hatua wanafunzi wa vyuo vikuu ambao wamekuwa wakiikosoa serikali waziwazi ,na hata wahadhiri ambao wamekuwa wakitumia taaluma zao kwa uwazi nakusema juu ya mapungufu ya serikali wachukuliwe hatua ya ama kufukuzwa kazi  au ajira zao kusitishwa. Hivyo hii ni muendelezo wautekelezaji wa maamuzi hayo. 


Nothing to stop you,just do it!!


 Nimesimama tayari kwa kuanza kufanya, lakini sijui nianzie wapi? Sio kama sijui  ninachotaka kukifanya, HAPANA!!nakifahamu fika ,tena akili  imelipangilia jambo hilo vizuri, tatizo macho yanaona lakini  hayaoni mwanzo wake!! Mikono na miguu ina nguvu lakini vimepatwa na kigugumzi haviwezi kufanya lolote!!  Chakusikitisha  domo langu gundi linashindwa kusema, ili nisaidiwe kuoneshwa mwanzo eti kisa nafsi inaogopa kuchekwa!  

   Hofu imezidi kuingia nafsini,  tena nazidi kuogopeshwa kwa lugha ya kizungu eti “time will tell” kwa tasfiri rahisi wanamaana eti nisubiri mpaka muda utakapozungumza! tangu lini muda ukawa na mdomo ?! tena sijui unazungumza lugha gani? Ghalfa nawakumbuka wahenga, wanananiambia “ngoja ngoja ya huumiza matumbo!” nami naingiwa na hofu ya kuumwa tumbo. Akili inazidi kufunguka na kuuona kuwa wakati ni ukuta, hivyo hakuna wakati mwingine wa kuyafanya haya. Muda ndo huu, akilini inakemea hofu, nguvu ya uthubutu inajaa nafsini, mara napokea muujiza, macho yanaona mwanzo mpya, mikono na miguu viko tayari kufanya kazi! Gundi lililojaa mdomoni linayeyuka ghalfa napata kusema, wengine wanadharau na kuona kile ninachotaka kufanya hakina maana, Sivunjiki moyo! wapo wanaonipa moyo nakuona uzuri wa kile ninachotaka  kufanya. Nainza safari ya kufanya, nilikuwa sioni mwanzo lakini sasa nauona. Safari inaendelea tena kwa mwendo wa LORUUU KEIKEI….sijali vikwazo vya njiani mpaka nitakapofika kwani siku zote “the end justify the means” kwani mwisho ndio utakaonipa majibu ya hiki ninachokifanya.

  Wengi tunateswa na ugonjwa huu,ni gonjwa la HOFU inasemekana wengi tunaugua ugojwa huu! mambo yetu mengi hayaendi kisa hofu, wengine stress (msongo wa mawazo) zinazidi kisa hofu. Dawa imegundulika kuwa ni kujipa moyo, uthubutu na kujiamini. Kataa hofu na if you want to do, DO IT NOW hakuna wakati mwingine.


Kila ufikiriapo ndipo mafanikio yako huongezeka!!!


Tukumbuke ndugu zangu,mawazo ndiyo mwanzo wa mafanikio yako. Unapokuwa na ndoto mafanikio kwanza yakupasa kuwa na wazo ambalo baadae utalifanyia kazi, ili utengeneze bahati yako. Kwa kufuata maelekezo hayo utakuza upeo wa fikra zako.

Wengi wanaweza wasikutendee haki, kama wengi wafanyavyo, wanaweza kukupotosha katika uhuru ulionao, lakini hawawezi kukuchukulia mawazo unayoyawaza. Kutokana na fikra zako utakuwa unashinda siku zote. 

Unataka kuwa na furaha? Unataka kuwa na amani? Unataka kuwa na cheo, nguvu au utajiri? Fikiri kuwa navyo, utafanikiwa. Fikra unazowaza ni muhimu kuliko ujuzi ulionao. 
Ujuzi una mipaka, mawazo yanatawala muda wote, yanaleta maendeleo. Kila mtu binafsi anakuwa na ndoto za mafanikio bila kujitambua. Kwa mfano, wazazi wanapopanga ni jinsi gani watawaendeleza watoto wao, wajasiriamali wanapopanga ni jinsi gani wataendeleza biashara zao hiyo yote ni mifano ya kuwa na ndoto njema ya mafanikio. Watu wachache wamejifunza kutumia mawazo yao kwa faida lakini wengi wetu mawazo tuliyonayo yanapata kutu kutokana na kutoyafanyia kazi. Hakuna sababu ya kuona aibu katika dunia ya ubunifu.

Kuwa na mawazo ya kufanya jambo fulani ni kitu kizuri katika dunia hii tunayoishi. Kila mmoja wetu ana kiwanda chake cha kuwa na mawazo. Lakini ni wapi mawazo hayo yanapotoka? Ni wapi waandishi, wana sayansi na wabunifu wanapopata mawazo makubwa? Kwa nini baadhi ya watu wengine wanakuwa wabunifu zaidi ya wengine? Ni kutokana na kutumia vizuri mawazo yao.

 Kila mmoja wetu, kwa wakati mmoja au mwingine, lazima kujifunza chanzo halisi cha mawazo. Utajiri, unaweza kuupata, inategemeana na ulivyoyaweka mawazo yako. Wazo dogo rahisi linaweza likabadilisha kabisa maisha yako uliyonayo.  Pia huwezi ukajua ukubwa wa mafanikio yako mpaka utakapojifunza jinsi ya kuchanganya juhudi zako na mawazo yako.  Kwa vyovyote unapotaka mafanikio unajitathmini wewe mwenyewe. Mwili uliopumzika una nguvu, vile vile akili. Kama unataka kuwa mbunifu na mpokeaji wa mawazo mapya, inakubidi kupata muda kwa mawazo hayo na kuyafanyia kazi.
Jizoeze kila siku kuwa na muda wa mapumziko, chagua chumba kizuri kilichotulia au kiti kizuri ambacho kitakusaidia kutuliza akili kwa urahisi. Unavyoendelea kujifunza kupumzika, utapata mawazo ambayo yatakufikisha katika malengo na matarajio yako.

Mtunzi anafikiri juu ya uimbaji, mchoraji anafikiri juu ya rangi, mwandishi anafikiri juu ya habari na maneno. Kama utachukua wazo moja na kulitendea kazi litakupa matokeo mazuri. Yafanyie kazi mawazo yanayokujia. Kuwa na utayari katika kunasa mawazo yako. Mawazo mengi mazuri yanapotea kwa sababu hayawekwi katika maandishi.

Tathimini mawazo yako. Mara tu unapomaliza kuyachuja mawazo yako, unachagua yale unayotaka kuyafanyia kazi. Utagundua kuwa nayo yanahitaji kuongezewa ubora wake. Jifunze ndugu yangu kutokufunga milango yako ya kuwa mbunifu.


Makala hii imetoka kwa Seif Kabele

UDPRSA 5th anniversary marked a new beginning!!

Celebration of the 5th anniversary of University of Dar es Salaam Public Relations Student Association (UDPRSA) has marked an opening way in which all UDPRSA members and other PR professional s in the industry to communicate and interact easily on matter concerning their career, this is due to the launching of their blog and face book page.

   While speaking to members the guest of honor and the main speaker his excellence Professor Eno Akipabio encourages leaders and members to be committed and insists leaders to come up with new ideas that will strengthen their association. He further said through such association will enable them to exchange their ideas, creating networks professionals and utilize the opportunities that face them as students. Prof Akipabio went on saying the opening of blog and facebook page is great achievement especially at this era of development of social and new media.
The display which shows UDPRSA blog
However, on his remarks Mr Amin Antony Mgeni who was among the founders of UDPRSA said he is happy to see the association still exists and he advise leaders to take quick solution to whatever challenge encounter the association. Mr Mgeni who is currently an editor at Mlimani tv, encourages members to use the blog in writing articles and feature stories hence would enable them to become good PR’s. 
On the left is Mr Kisoma Mussa and Mr Amini Mgheni one of the founder of UDPRSA
“This 5th anniversary is a challenge to me and my cabinet, we ensure that UDPRSA will still move on, but without your cooperation (members), UDPRSA won’t succeed” said the new President of UDPRSA, Mr Kisoma Mussa. He added that up to this time they succeed to create a network with association like University of Dar es Salaam Markerting Association (DUMA), Saut Student Public Relations Association (SSPRA) and currently they are in discussion with Public Relations Association of Tanzania to see on how they can work together.

From the left is UDPRSA vice president Mr Raymond,Bonnie-UDPRSA deputy GSProf  Akipabio and Kijanga
The 5th anniversary celebration was held on 10th November at School Journalism and Mass Communication and was attended by the Director of Publicity at DUMA, Mr Enock Ngulwa, media people and other alumni of SJMC.
UDPRSA members during 5th anniversary event.

HATUWEZI KUENDELEA KWA NCHI ILIYOJAA WANYOA VIDUKU!!

  Nafurahishwa sana kwa kuona muamko mkubwa wa Watanzania wengi  kutaka kuwa na maendeleo katika nchi yetu, hamasa hii inatokana  na kufunguka kifikra na kiakili miongoni mwa watu hivyo kupelekea kujitambua na kujua haki zao na kipi wa wanachokitaka  kiwepo katika jamii yetu. Lakini kwa masikitiko makubwa napenda kuwa vunja moyo kwa kuwaambia kuwa HATUWEZI kupata maendeleo kwa taifa lililojaa wanyoa viduku na wavaa supra!!” .   Najua unajiuliza kwani kuvaa supra na konyoa kiduku  kuna mahusiano gani na suala la maendeleo?? Sina  maana ya wazi kiiivo ,naamanisha kuwa suala la maendeleo hushangiwa kwa kiasi  kikubwa na kupevuka kwa fikra kwani hata Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa” Umasikini wa fikra ni umasikini mkali kuliko yote” lakini wengi wetu hasa vijana bado hatujataka  kuzipevua akili zetu bali tumezidi kuzidumaza fikra zetu kwa kufikiria kunyoa viduku,kuvaa  kata K, huku tuikimba Muhogo andazi, Muhogo andazi, na kwa sauti kubwa tunaimba ni sababu ya Ulofa na nyimbo nyingine za mahadhi hayo. Zaidi ya hapo tunafikiria ni lini tutaenda kupiga picha za editing kule my fair au photo point! Kubali kataa hayo ndio mawazo ya sisi vijana wa leo. Mfano mzuri ni wengi wa wanamuziki wetu vijana hawatoi nyimbo zenye hamasa kwetu.

KATIKA HILI WATANZANIA TUMEMSAHAU GADDAFI!!

  Inaelekea waTanzania wengi wamesahau historia kati ya Libya na Tanzania. Marehemu Gaddafi alikuwa rafiki yake mpenzi nduli mshenzi Dikteta Idi Amin Dada wa Uganda!  Gaddafi alitaka Amin amwoe binti yake! Gaddafi alituma wanajeshi kutoka Libya kuwasaidia Uganda katika vita vya Kagera mwaka 1978-79.  Sisi wazee tunaikumbuka hio vita na miezi kumi na nane (miaka 18) ya shida iliyofuata!  Maoni chini yameandikwa na mwanachama la kundi - Wanabidii

Kanali Gaddafi alipotembelea Uganda mwaka 1978

...Wanabidii!


  
Binafsi nachukia sana kuandika bila ya ushahidi! Na zaidi sipendi kuandika "propaganda" na taarifa za uzushi; isipokuwa napenda kuandika taarifa zilizotafitiwa kwa kuandikwa na mtafiti mwenyewe (na au mwandishi aliyeandika matokeo ya utafiti au kufanya upembuzi wa utafiti husika). Takriban wiki moja sasa (tangu Alkhamis ya tarehe 20 Oktoba, 2011) uwanja wa "Wanabidii" na majukwaa mengine ya kijamii yamekuwa yakijadili "Kuuawa kwa Kanali Muammar Gaddafi" kulikofanywa na wale wanaoitwa waasi (wa NTC) wakisaidiwa na NATO wakiongozwa na Uingereza, Marekani, Ufaranza na washirika pamoja na Waarabu (Saudia na Qatar). Gaddafi ameuawa; kwa jinsi gani, kila mmoja amesoma, ameona (kwenye picha za mndato) na au kwenye picha za video!

  
Ninachotaka kuandika na pengine kuanzisha "mjadala" wa kiakili ni juu ya "GADDAFI KUMSAIDIA IDI AMIN DADA KWENYE VITA VYA KAGERA [UGANDA DHIDI YA TANZANIA MWAKA 1978 HADI 1979]". Napenda niweke wazi kwamba, "historia haisomwi ili kufufua 'chuki' bali husomwa kujua yaliyopita, kuyasanifu yaliyopo na kupanga mipango kwa yajayo!". Hivi ndivyo tunavyosoma historia iwe yenye kuhuzunisha au kufurahisha! Tanzania ilipigana vita na Uganda, vita iliyoitwa VITA YA KAGERA (japokuwa ilipiganwa hata ndani ya Uganda na Idi Amini Dada kufurushwa na kuikimbia Uganda!).

Kwa ujumla, tangu pale kifo cha Muammar Gaddafi kilipotangazwa kwa mara ya kwanza na kituo cha runinga cha Al-Jazeera na kukaririwa na vituo vingine na mashirika ya habari ya kimataifa kama BBC, CNN, Reuters, Xinhua, AFP, AP na IRNA (Press Tv) kumekuwa na mkanganyiko wa "mawazo" kwa wananchi wa Tanzania juu ya "hali" ya Gaddafi kisiasa katika mtazamo wa kifalsafa...hususan wengi wa wachangiaji kwenye mijadala hiyo wanamuona Muammar Gaddafi kama "shujaa" na "mwanamapinduzi" na "kiongozi mtukuka" na "aliyejitolea kuunganisha Afrika" na hata wengine kufikia kiasi cha kuonyesha kwamba hajawahi kutokea kama Muammar Gaddafi na hata kumpa "daraja" ya kuwa "Baba wa Afrika" na mshumaa uliyozimika! Hata hivyo wengi wamesahau kwamba ni Muammar Gaddafi ndiye aliyemsaidia Idi Amin Dada kwenye Vita vya Kagera! Naomba sasa tuangalie nini alifanya Gaddafi wakati wa vita vile.

Vita vinahitaji rasilimali watu (askari na wataalamu wa kijeshi), fedha za kuendeshea vita na zana (za kivita na za mawasiliano ya kivita). Kwa mujibu wa taarifa rasmi na zinazothibitishwa na taarifa rasmi za kihistoria Muammar Gadafi alimpa Idi Amin Dada usaidizi ufuatao:

HOTUBA YA MBUNGE WA MONDULI, EDWARD LOWASSA KWA WAANDISHI WA HABARI OKTOBA 19, 2011

Ifuatayo ni hotuba ya waziri mkuu mstaafu amabaye pia ni mbunge wa Monduli muheshimiwa Edward Lowassa aliyoitoa mapema leo nyumbani kwake Monduli Arusha, wakati akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari…….

    NDUGU wana habari nimewaita katika mkutano huu leo kwa sababu moja kubwa, kutoa ufafanuzi kuhusu matukio ambayo yamekuwa yakitokea huku yakinihusisha mimi binafsi kwa namna ambayo sasa yanatishia ustawi na mshikamano wa kimaadili, kihistoria na kikazi miongoni mwa viongozi na baina ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

    Ndugu wana habari, naamini mmekuwa mkifuatilia kwa karibu habari zinazoripotiwa katika baadhi ya vyombo vya habari zinazolihusisha jina langu na harakati kadha wa kadha chafu ambazo hata mimi mwenyewe ninayehusishwa nazo huwa nazisikia na kuzijua baada ya kuwa zimesharipotiwa katika vyombo hivyo vya habari.

  Uamuzi wangu wa kukutana nanyi leo hauna makusudi ya kuzozana na vyombo vya habari wala kwenda kinyume na utamaduni wa kimaadili wa ndani ya chama changu unaotutaka viongozi kujadili masuala yanayokihusu chama chetu ndani ya vikao vyetu rasmi vya kimaamuzi bali kutoa ufafanuzina angalizo kwa pande zote hizo mbili ambazo zinaguswa na matukio yanayoendelea kutokea leo hii.

  Moja ya mambo ambayo yameligusa jina langu kwa namna hiyo ni lile linalonihusisha eti na kundi moja la wanasiasa ambao wamekuwa na mikakati ya kumhujumu mwenyekiti wetu wa chama, Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete. Hakuna shaka ni madai ya kipuuzi, kizushi na yenye malengo machafu.

  Hawakuishia hapo sasa wamefikia hatua ya kuvitumia vyombo hivyo hivyo vya habari na kufikia hatua ya kudai kwamba nimeanza kuandaa orodha ya kile wanachokiita madhambi ya Rais Kikwete ambayo wanadai nimepanga kuyasoma wakati wa kikao kijacho cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (CCM).

  Ninaamini kwa dhati kabisa kwamba, waandishi wa habari wanaofuatilia kwa karibu na kwa umakini mwenendo wa masuala ya kisiasa nchini wanatambua kwamba, watu wanaopenyeza taarifa hizi katika vyombo vya habari wanafanya hivyo kwa malengo ya kufikirika ya kujisafishia njia kisiasa.

  Ni jambo lisiloingia akilini kunihusisha na kile kinachoitwa mikakati ya kumhujumu rais 

Our time to say Goodbye

    Jana was happy, great and unforgettable day to all Jitegemee form four students because they were saying kwaheri (graduating) kwa walimu na wanafunzi wenzao  walioishi nao kwa miaka minne hapo shuleni kwao.
Baadhi ya wanafuzi wakiwa katika pozi
Mdau Edo (kushoto) ni mmoja wa wahitimu
Wote walikuwa na furaha huku wakionesha  hamu ya kuingia kidato cha tano.

Poziiiiii!!
     Sherehe hiyo ilifanyika shule hapo maeneo ya Kurasini kilwa road,kulikuwa na burudani zilizotolewa na wanafunzi wenyewe na vituko kama kawaida havikukosekana.
Mshikaji akihuzunika kwa kumaliza chakula chake!!
Big aking'ang'ana na kipapatio cha kuku!!
  Wanafunzi wote wamefurahia kuhitimu elimu ya sekondari na wanaomba uzima na nguvu ilikufika tarehe 3 october na waweze kufanya mitihani yao salama. Pia wameshukuru kwa sherehe hiyo kufanyika kabla ya mitihani kwasababu itawasaidia kupunguza stress na hofu ya mtihani.
May GOD BE WITH YOU ALL FORM FOUR STUDENTS & ALL THE BEST KATIKA MITIHANI YENU HAPO TAREHE 3.

MAOMBOLEZO TANZANIA

Kufuatia msiba ulioikumba Tanzania kutokana na ajali ya boti ya MV Spice Islander iliyotokea katika eneo la Nungwi katikati ya bahari ya Hindi, Serikali  imetangaza siku tatu za maombolezo kuanzia leo tarehe 11,hivyo bendera itapepea nusu mlingoti kuashiria maombolezo hayo. Halikadhalika serikali imeridhia kuzika miili ya maiti zote ambazo hazitatambulika. Kutokana na ajali hiyo,imethibitika  takribani watu 192 na wengine zaidi ya 600 wameokolewa.  Taarifa za awali zinaonesha chanzo cha ajali hiyo kuwa ni kubeba  abiria na mizigo  mingi zaidi ya uwezo wake. Kwa upande wao jeshi la Polisi nchi limeunda  za uokoaji wa majeruhi na kuchunguza  chanzo cha ajali hiyo.
Viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wakitoa heshima kwa marehemu.

Rais Kikwete akiangalia miili ya vichanga waliofariki katika ajali hiyo.
Miili ya marehemu ikisuburi kutambuliwa na ndugu zao


Hii ni ajali kubwa ya kwanza kutokea katika mwambao wa Zanzibar. Modreamz inatoa pole kwa wote walioguswa na msiba huu MUNGU AZILAZE  ROHO ZA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI.

                                                                                                                         pic from jikumbuke blog

Salha Israel,the new Miss Tanzania 2011.

   Shindano la Vodacom Miss Tanzania limemalizika kwa Salha Israel kuibuka mshindi na kutwaa taji hilo kwa mwaka 2011.Washindi wengine ni Tracy Sospeter kutoka Shinyanga aliyeshika nafasi ya pili na Alexia William kutoka Kinondoni aliyepata nafasi ya tatu.
Miss Tanzania 2011 Salha Israel (katikati) akiwa na washindi wengine Tracy Sospeter (kulia) na Alexia William (kushoto)
Kufuatia ushindi huo Salha ataiwakilisha Tanzania katika shindano la urembo duniani ( Miss World 2011).All THE BEST n TAKE CARE COZ EVERY EYES ARE ON YOU.
Salha Israel Miss Tanzania 2011 akivishwa taji lake

You are beautiful in your color!!

Nikiwa katika mihangaiko ya kazi nikaenda kwenye ofisi moja maeneo ya Ubungo. Nilipokelewa na mama mmoja (mlinzi) wakati ananipa utaratibu nilikuwa na mshangaa kwa masikitiko kwa jinsi alivyoharibika uso wake (kaungua na kuweka ukungu mweusi). Kwa nyakati hizi imekuwa kawaida kukutana na watu wa aina hii wengine utawakuta ni weupe kupitiliza, wengine wekundu, wengine wamebabuka yaani balaa tupu! sio tu akina dada bali hata akina kaka nao wamejiingiza katika matumizi ya Creams.
Moja ya wanawake walioharibika kutokana na matumizi ya vipodozi pic by modernghana

      Creams ninazozitahaja hapa ni lightening (bleaching) creams ambazo zime-contain mercury and hydroquinone, alpha hydroxyl acids, Arsenic,na nyinginezo nyingi.Kutokana na utafiti wa Dr S Allen Counter 2003 ilionekana kuwa sumu ya mercury (zebaki) imekutwa kwenye miili ya watu wengi wao wakiwa wanawake. Nchi zilizooneka kuwa vinara katika hili ni Mexico,Saudi Arabia, Senegal,Tanzania na nchi nyingine za Afrika magharibi. Sababu kubwa unayowafanya watu kuji-cream (kujichubua) ni kwa ajili kwa kutaka kuonekana warembo. Lakini hii ni kasumba mbaya kwani kuwa mrembo au kuonekana unapendeza ni lazima uwe mweupe? HAPANA tena tafiti zinaonyesha kuwa most beautiful and attractive women in the world are actually black women! Angalia akina Naomi Campbell, Halle Berry, Tyra Banks,Miriam Odemba, Nancy Sumari na wengine wengi. Kibaya zaidi tunaambiwa “Beauty is more than skin deep” . Athari kubwa zimekuwa zikionekana sana huku kwetu Afrika kwa sababu vipodozi hivi vingi haviko favorable na mazingira yetu kwani watngenezaji wanashauri watumiaji wasiwe wanakaa jua au watumie sunblock masharti haya wengi wa akina dada zetu yamewashinda!! Hivyo kujikuta wanababuka ngozi zao,  athari nyingine ambazo zinazowatokea ni kuzeeka kwa ngozi kutokana na mikunjo hivyo kumfanya kijana anaonekane mzee, kupata cancer hali kadhalika kifo chaweza kutokea kwa wale wanaofanya  plastic surgery.
Nancy Sumari one of the black beautiful girl
  Licha ya vipodozi hivi kupigwa marufuku katika nchi mbalimbali lakin bado vimekuwa vikiuzwa  kinyemela.Imeshauriwa kuwa watumiaji waepuke vipodozi vyenye chemical hizo au watumie vipodozi vya asili (HERBAL) ambavyo vinaweza kulinda urembo wao.
Jikubali ulivyo because you are beautiful in your natural color.

VOTE FOR Mt KILIMANJARO


   Ukiwa kama mdau wa unahimizwa kuuwezesha mlima Kilimanjaro kushinda na kuwa moja ya maajabu ya dunia. Hii ni kupitia shindano la new 7 world wonders linaloendeshwa hivi sasa. Mlima Kilimanjaro una mita 5895 kutoka usawa wa bahari  (5895 from the sea level)  una vigezo vyote vya kuingia katika  new world wonders, kwanza   kabisa ni mlima mrefu kuliko yote barani Africa, pia una vilele viwili ambavyo ni Kibo na Mawenzi zaidi ni kwamba, inastaajabisha kwa mlima kama huu (Volcanic mountain)  kuweko katika ukanda wenye hali ya hewa ya Kitropiki.
 Kuupigia kura ni rahisi tembelea www.new7wonders.com au bofya  hapahttp://www.new7wonders.com/vote-2?lang=en
      Lets unite & enable mount Kilimanjaro to be the new world wonder.