Tamko la BAVICHA kuhusu wanafunzi waliofukuzwa vyuoni.

       Kwa miaka ya hivi karibuni Vyuo mbalimbali vimekua na tabia yakuwafukuza ama kuwasimamisha masomo wanafunzi wanaoendelea na masomo kwenye vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini mwetu kutokana na mashinikizombalimbali kutoka kwa viongozi wa kiserikali kwa kisingizio kuwa wanafunzi hawa wanafanya siasa vyuoni.Itakumbukuwa kuwa migomo na maandamano ya wanafunzi kwa vyuo vikuuhapa nchini haijaanza pale mfumo wa vyama vingi uliporuhusiwa kuanzamwaka 1992 ,bali migomo na maandamano haya yamekuwepo tangu kuanzishwa kwa vyuo hivyo.Mathalani, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimekuwa na historia ya migomo na maandamano ya mara kwa mara tangu kuanzishwa kwake , na hivyo dhanaya kuwa wanafunzi wanagoma kutokana na misukumo ya kisiasa sio sahihihata kidogo bali ni mbinu ya watawala kujaribu kuficha madhaifu yao .Wanafunzi hawa wamekuwa wakigoma kutokana na serikali ya CCM kuendeshamambo yake kibabe na kwa dharahu ya hali ya juu ambapo imefanya elimukuwa Privilage na si haki kwa watanzania.

Kwa mantiki hiyo basi, kutokutendewa haki kwa wanafunzi hawa naserikali yao, kukosekana kwa miundombinu bora ya kusoma na kujifunzia,wanafunzi hawa kunyanyaswa na watawala wa vyuo hivyo, kukosekana kwamikopo kwa wakati muafaka, serikali kuingilia uendeshaji wa vyuo ,serikali kuvunja serikali za wanafunzi bila kutoa sababu za kimsingi na sababu nyingine mbalimbali ndio chanzo cha vurugu na migomo vyuoni.

Hivyo basi , kutokana na sababu tajwa hapo juu Baraza la Vijana na CHADEMA (BAVICHA) tunatamka wazi kuwa kitendo cha Vyuo Vikuu vya Dar Es Salaam, Dodoma na Muhimbili kuwafukuza wanafunzi kwa ujumla wakez aidi ya 100 ni kitendo cha uonevu kwa wanafunzi hawa na kamwe hakivumiliki hata kidogo na haswa ikizingatiwa kuwa ni watoto wa watu masikini na ambao kimsingi wanajilipia ada wenyewe kwani wanakopa na baada ya muda watapaswa kulipa fedha hizo.
Kwa nini tunapinga uamuzi huu wa kuwafukuza wanafunzi vyuoni;
 
1. Ni kinyume na Tamko la Ulimwengu la mwaka 1990 la uhuru wa kitaaluma (Academic Freedom) ambalo tulisaini mnamo mwezi April tarehe29 hapa Dar Es Salaam , linasema wazi kuwa ni lazima Vyuo vijiendeshe kwa uhuru kamili bila kuingiliwa na serikali .
2. Kufukuzwa kwa wanafunzi hawa ni utekelezaji wa Maazimio ya vikaovya CCM vilivyofanyika na haswa vile vya Halimashauri Kuu ambavyo vimetoa maelekezo mbalimbali kwa Serikali juu ya kuwachukulia hatua wanafunzi wa vyuo vikuu ambao wamekuwa wakiikosoa serikali waziwazi ,na hata wahadhiri ambao wamekuwa wakitumia taaluma zao kwa uwazi nakusema juu ya mapungufu ya serikali wachukuliwe hatua ya ama kufukuzwa kazi  au ajira zao kusitishwa. Hivyo hii ni muendelezo wautekelezaji wa maamuzi hayo.