MATUKIO YALIYOJIRI TANZANIA 2012# karibu 2013



Ugonjwa wa Dk. Mwakyembe  Januari 3, 2012
HALI ya afya ya Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe, ilikuwa inasikitisha kwani licha ya kupata matibabu nchini India na kuendelea na tiba hiyo hapa nchini, hali yake haikuwa ya kuridhisha kutokana na kunyonyoka nywele, kope, ndevu na vinyweleo vyote.

Madaktari 229 wafukuzwa Muhimbili Januari 6, 2012
UONGOZI wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) uliwafukuza kazi madaktari 229 waliokuwa katika mafunzo kwa njia ya vitendo kutokana na mgomo wa siku nne wakishinikiza kulipwa posho zao za mwezi mmoja.

Umeme bei juu Januari 14, 2012
WAKATI gharama za maisha kwa Watanzania wengi zikizidi kupanda kila siku, Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), iliidhinisha ongezeko la bei ya umeme kwa asilimia 40.29 kwa Tanzania Bara na asilimia 28.21 kwa Zanzibar kuanzia Januari 15, 2012.
Madaktari waanza mgomo nchi nzima Januari 23, 2012
JUMUIYA ya Madaktari Nchini, ilianza mgomo nchi nzima hadi pale ambapo serikali ingeliridhia kulipa madai yao ndipo madaktari wangelirudi kuendelea na kazi.
Mwenyekiti wa Kamati ya Madaktari, Dk. Ulimboka Stephen, alisema mgomo huo ungelikuwa wa nchi nzima kwa madaktari kutotoa huduma.



Wanafunzi wanane wafa maji Arusha Februari 28, 2012
WANAFUNZI wanane kati ya kumi wa Shule ya Msingi Piyaya, wilayani Ngorongoro, mkoani Arusha, walifariki baada ya kusombwa na maji ya mafuriko ya Mto Radiru wakati wakitoka shuleni, jioni majira ya saa 11:30.

Mei 3, 2012 Watu saba wafa ajali ya basi la NBS
WATU saba walikufa papo hapo na wengine 54 walijeruhiwa baada ya basi la kampuni ya NBS lenye namba za usajili T 978 ATM lililokuwa likitokea Tabora kuelekea Arusha kupinduka katika eneo la Jineri, nje kidogo ya mji wa Igunga.

Dk. Ulimboka atekwa na kupigwa Juni 28, 2012
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk. Steven Ulimboka, alitekwa na watu wasiojulikana, kupigwa na kujeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili, kisha kutupwa katika msitu wa pande, nje kidogo ya jiji Dar es Salaam.


Serikali yawashtaki madaktari Julai 7, 2012
SERIKALI iliwashtaki katika Baraza la Madaktari Tanzania, madaktari wanafunzi wa vitendo walioshiriki kwenye mgomo wa madaktari uliofanyika nchini kwa tuhuma za kuhatarisha maisha ya wagonjwa na kukiuka maadili ya taaluma yao.

Meli ya Mv Skagit yazama Julai 18, 2012
Kisiwa cha Zanzibar kilikumbwa na msiba mzito kutokana na kuzama kwa meli ya MV Skagit, mali ya Kampuni ya Seagull, iliyokuwa ikisafiri kutoka Dar es Salaam ikiwa na abiria wanaokadiriwa kuwa 290 pamoja na mizigo kuelekea Unguja, visiwani Zanzibar majira ya saa saba mchana. Watu 63 walifariki, 146 wakiokolewa hai na 81 hawakupatikana.


Sheria ya mifuko ya jamii moto Julai 27, 2012
VUGUVUGU la kupinga mabadiliko ya sheria za mifuko ya hifadhi ya jamii ya mwaka 2012 lilichukua sura mpya baada ya wabunge kutaka kuifanyia marekebisho mengine kwa sababu mwanachama hataruhusiwa kuchukua mafao yake kwa sababu yoyote mpaka hapo atakapofikisha miaka 55 au 60.

Ugonjwa wa ebola waingia nchini Agosti 5, 2012
UGONJWA hatari wa ebola ambao umeua idadi kubwa ya watu nchini Uganda uliripotiwa kuingia nchini katika wilaya ya Kyerwa, kijiji cha Bulongo, mkoani Kagera, ambapo mtoto wa miaka sita alionekana na dalili hizo.

Walimu watishia kuing’oa CCM Agosti 6, 2012
WALIMU walipokubali kurejea kazini na kuendelea kutafakari amri ya mahakama, mkakati mzito ulipangwa kuhakikisha hawakiungi mkono Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.

Mauaji ya Daudi MWANGOSI Septemba 3, 2012
Jeshi la Polisi lilimuua mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Channel Ten, Daudi Mwangosi, aliyekuwa anaripoti habari za ufunguzi wa matawi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), mkoani hapa.
Mwangosi alidaiwa kuuawa kwa bomu lililorushwa na polisi waliotaka kuizuia CHADEMA kufungua tawi katika kijiji cha Nyololo.

Waislamu waandamana Dar Septemba 21, 2012
MAELFU ya waumini wa dini ya Kiislamu waliandamana na kukusanyika kwenye viwanja vya Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam ambako walitoa tamko dhidi ya wanaoshambulia na kunyanyasa Uislamu, hasa kwa Marekani kutengeneza filamu ikimkashifu Mtume Muhammad (SAW).

Ajali yaua 10 Mbeya, mbunge anusurika Oktoba 3, 2012
MBUNGE wa Viti Maalum Mbeya kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Mary Mwanjelwa, alinusurika kufa katika ajali iliyogharimu maisha ya watu takriban 10.
Ajali hiyo ilitokea eneo la Mbalizi, wilaya ya Mbeya Vijijini. Gari la mbunge huyo liligongwa na kuteketea kwa moto papo hapo.

Kizaazaa cha mafuta Dar Oktoba 3 2012                     
MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) baada ya kushusha bei za mafuta ya petroli na dizeli nchini, baadhi ya wafanyabiashara walizua kizaazaa kwa kuweka mgomo baridi wa kuuza mafuta hayo.



 Waislamu wachoma, wavunja makanisa Oktoba 12, 2012
KUNDI kubwa la Waislamu wenye imani kali, lilizusha vurugu kubwa zilizoambatana na kuchomwa moto na kuharibiwa makanisa manne huko Mbagala jijini Dar es Salaam, katika kile kilichoelezwa kuchukizwa na kitendo cha kijana mmoja wa Kikristo aliyedaiwa kukimwagia haja ndogo kitabu kitakatifu cha Kurani.

Ponda akamatwa kwa uchochezi Oktoba 17, 2012
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, lilimtia mbaroni Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Sheikh Issa Ponda Issa, akikabiliwa na tuhuma mbalimbali za uchochezi.









Padri apigwa risasi Zanzibar Desemba 26, 2012
PADRI wa Kanisa Katoliki lililoko Mpendae visiwani Zanzibar, Ambrose Mkenda, alijeruhiwa kwa risasi na watu wasiojulikana nje ya nyumba yake majira ya saa 12 jioni  wakati akitoka kanisani.

Che Mundugwao arudi na Kandindi





Baada ya kukaa kimya kwa miaka miwili, mwanamuziki wa miondoko ya Asili, Che Mundugwao a.k.a Mtoto wa Lulindi ametoa nyimbo yake mpya inayoitwa KANDINDI. Akizungumza na modreamz, Che Mundu amesema KANDINDI, inazungumzia maisha yake halisi ya wakati akirudi nyumbani kwao Lulindi Masasi na  mchanganyiko wa ladha ya asili na ladha ya mziki wa sasa (Bongo Beats). Ameongeza kuwa nyimbo hiyo ameimba kwa lugha ya Kiyao kwani hata jina lenye lina maana ya ndege aitwae Mdiria au King fisher kwa Kiingereza. Halikadhalika Che Mundu amesema nyimbo hiyo itakata kiu ya mashabiki wake waliokua wakimsubiri kwa muda mrefu.

How can a young researcher come up with accurate data



By  ADAM GAMBA
 
There are claims that often emerge regarding to young Researchers in developing countries mainly here in Tanzania that our researchers do not collect enough data when it comes to the issue of dissertation and other assignments which need collection of information.
This problem has been prevailing now and then especially among young researchers who work hard looking for experience and those who conduct research as their partial fulfillment for their degrees or accomplishing certain programs as well.
As long as these young researchers show increasing need for certain valuable information for their projects, they experience some difficulties from other individuals and in various institutions.
Unfortunately, these difficulties are not only found in small size institutions but also even in big and very important ones and sometimes even those which deal with the same research activities. This happens in both public and private offices.
 It is difficult to understand what bring about such situation into many places. Is it due to laziness, ignorance and lower thinking capacity, or abnormal behavior of some people, misconception, or the nature of the given society?
The most terrifying thing is that these happen even in bigger and higher learning institutions, like universities, colleges and different schools which we do consider to be most helpful to people in these academic matters.
Actually, there is no development without the work of researchers, because researchers are the one who inspire changes. In order to investigate problems, people should conduct researches which may reveal how the whole issue and how can be solved for, development to be achieved easily.
 As for, we journalists, we believe that “NO RESEARCH NO RIGHT TO SPEAK” so how can we be able to speak if  all people and various officers from whom we need information from them will not be ready to participate in providing such information?
ACTUALLY, this happened to me once or twice by the time I conducted certain project. When distributing questionnaires people received them with great joy. But  Problems arose by the time for data collection, whereby nearly half of the respondents had not completed  filling  many questions, some of them did not attempt even a single questionnaire whilst others kept on promising;” We will fill them don’t worry.”
Let us think of this, is it fair for these big and respected institutions to keep on promising young researchers day by day?
Keeping on saying; ‘come tomorrow, then tomorrow while others failing even to read the questions and  some individuals keep on complaining  that their bosses were not present for and so  they failed to submit the task to the respected persons. I do not know whether the bosses do nowadays move with their offices wherever they go. 
These are our intellectuals; some are research experts, heading huge research institutions here in Tanzania while they fail to provide information to their young researchers in spite of knowing the significances of the research projects in the world.
It is wonderful! Wonderful indeed, how comes the researchers deny other researchers the opportunity to do research; they reject to give information and share experiences for bringing development. How will these young researchers gain experience and like going to the field to search for data, if at all the experts are not ready to provide valuable information required for certain project?
 By the end of the project I came to realize that, that is why people from developed nations do sometimes doubt our findings simply because of this tendency that has been implanted in many individuals in Tanzania and other parts of East Africa. Because they fear that may be these researchers, after having a lot of setbacks, can even decide to cook data in order only to accomplish the project in time.
This conclusion came about after my research leader who went to collect data in Burundi and Rwanda, encounter some difficulties in Burundi, as not even a single questionnaire was attempted.
Come on! Africa, is it because of only being black, ignorant, poor or leading serious less?