THE GAME NDANI YA KIJOGOO

Msanii The Game nae ameamua kutupia style ya Kijogoo a.k.a  KIDUKU kwenye kichwa chake.Style hii hapa nchini inapendwa sana na wasanii kutoka THT

VIKOMBE VYAZIDI KUTOLEWA!!!

Baada ya Mchungaji mstaafu Bw Ambilikile Masapile"BABU" kuja na dawa inayotibu magonjwa sugu "KIKOMBE" kaoteshwa na MUNGU.Sasa kumeibuka watu wengine wanaogawa dawa kwa mtindo huo wa KIKOMBE nao wanadai wameoteshwa!!

Babu akifanya vitu vyake.
Mfano huko Tabora amejitokea mwanamke anaetambulika kwa jina la Magret Mutalemwa a.k.a BIBI nae anagawa kikombe kwa madai kuwa ameoteshwa na Bikira Maria,tofauti na BABU,BIBI anatumia kikombe cha udongo huku akikushika kichwa wakati anakupa kikombe.Wagonjwa mbalimbali wametoa shuhuda za kupata nafuu baada ya kupata kikombe cha Bibi,huku wakiitaka serikali kupitia halmashauri ya Tabora kumsaidia BIBI kutoa huduma hiyo kwani mazingira ya kufika kwake sio mazuri.
                              bibi na kikombe chake.

Halikadhalika huko Pwani maeneo ya Ruvu Darajani amejitokeza kijana Juni Abunda aliyepewa jina la KAKA,nae anagawa kikombe kinachotibu magonjwa sugu kwa madai ya kuoteshwa na Mungu.Kaka yeye anatoa kikombe bure!!!
Wakati huohuo ahuko Mbeya Mchungaji Mwasumale wa kanisa la kinabii lililopo Tukuyu Rungwe nae anatoa kikombe.Mbali na hao Morogoro nako amejitokeza mwanamke mwingine anayeitwa Fatma Senga nae anagawa kikombe.Sasa sijui huyu ataitwa nani?? labda Shangazi.