UHURU WA HABARI TANZANIA #Hekaya za Ray Mtani

Na Raymond Mtani
Leo ni siku ya uhuru wa habari dudiniani, lengo kuu la maadhimisho ya siku hii may 3, (world press freedom day) ni:

• kukuza uelewa kuhusu umuhimu wa uhuru wa habari na
• kukumbusha serikari wajibu wake wa kuheshimu na kuthamini haki ya uhuru wa kujieleza kama unavyotajwa katika Ibara ya 19 ya mkataba wa haki za binadam.

Labda kwa faida ya jumla Ibara ya 19 ya mkataba wa kimataifa wa haki za binaadam inasomeka hivi “Everyone has the right to freedom of opinion and expression; the right includes freedom to hold opinions without interference and to seek, receive and impart information and ideas through any media regardless of frontiers”

Kila mtu anao uhuru wa kuwa na maoni na kueleza fikra zake; anayo haki ya kutafuta, kupokea na kutoa habari bila kujali mipaka. Zaidi tafsiri ya Ibara hiyo imehuishwa katika ibara ya 18 ya katiba ya JMT 1977 na mabadiliko yake ya mwaka 2005.
Kwangu mimi siku hiyo ni zaidi ya muhimu kwa ustawi wa demeokrasia ya nchi yetu, ni muhimu kwa ajili ya kuhamasisha na kuchochea mawazo mbadala, hasa ikizingatiwa kuwa mwaka huu waandishi na jamii ya wapenda haki za binadamu wanaadhimisha siku hiyo kukiwa na kumbukumbu ya matukio mabaya kupata kutokea katika historia ya nchi yetu,

Naam nitataja machache, mosi ni mauaji ya kinyama ya mwandishi Daudi mwangosi akiwa kazi kutafuta habari kama ibara ya 18,(b) ya katiba ya JMT inavyompa haki hiyo. Ipo kumbukumbu ya Mwenyekiti wa jukwaa la wahariri kutekwa, kuteswa, kung’olewa kucha, jicho na kasha kutelekezwa hadi leo hii yungali anauguza majeraha huko Afrika kusini.

Vile vile tunaadhimisha siku hiyo kukiwa na kumbukumbu ya kutekwa, kuteswa, kungolewa kucha, meno na kutelekezwa katika msitu wa Pande kwa mwanyekiti wa jumuhiya ya mdaktari nchini Dr steven Olimboka, huyu alikuwa katika harakati za kukuza uhuru wa kujileza(haki ya msingi ya kikatiba)

Kama hiyo haitoshi ni hivi juzi may 1, mkuu wa mkoa wa Arusha alitishia waandishi wa habari akiwataka kuwa makini pindi wanapoandika habari zinazohusu migogoro ya viongozi akienda mbali zaidi na kudai roho zao zitakua mkononi

"Unapoingia katika mkakati wa kudhalilisha kiongozi wa serikali unakuwa umeiweka roho yako rehani, kuweni makini" alisema Magesa Mulongo mkuu wa mkoa wa Arusha katika maadhimisho ya siku ya wafanya kazi duniani.

Tunaadhimisha siku hii kukiwa na jaribio la Bunge kuzuia vyombo vya habari kurusha matangazo yake ya moja kwa moja ingawa jaribio hilo linaonekana kushidwa juhudi zingali zinafanywa hii ni kutokana na kiongozi mkuu wa bunge Speaker Anne Makinda kurudia mara kwa mara kuwa hawafanyi kazi taarifa za vyombo vya habari.

Mbali na msululu wa sharia mbovu zinazonyima waandishi na vyombo vya habari kwa ujumla kufanya kazi zao kwa weledi kwa kutoa taarifa zenye ushahidi wa kina, serikali imekuwa ikitumia lungu la sharia hizo mbovu kushitaki waandishi na kufungia kila chombo cha habari kinachokinzana na matakwa yake, wote tunakumbuka tukio la kufungiwa kwa gazeti la MWANAHALISI.

Orodha ni ndefu sana, yatosha kusema kila mtanzania kwa nafasi yake anawajibika kushinikiza serikali hii kuheshimu uhuru wa habari, kujieleza ni haki pekee ya msingi, siyo matakwa ya mtu bila kuwa makini kupitia haki hii tutaibiwa, tutanyanyaswa, tutateswa na kufanyiwa kila hila.
Namaliza kwa kusema ni rahisi sana kumuua mtu kuliko kumyamazisha kusema.