WANAWAKE HAWA JAMANI!!




Inashangaza kuona wanawake hawa kunyonyesha wanyama.!!

MPAKA KIELEWEKE!!

"Kitafahamika tu!!" Hayo ni maneno ya Binti wa Kijerumani Regina Mayer, ambaye kwa muda mrefu alikuwa na ndoto ya kuendesha farasi lakini haukweza kufanikiwa kwa wazazi wake hawakumwezesha kutimiza ndoto zake. Basi ndipo binti huyo wa miaka 15 alipoamua kumfundisha ng'ombe wake aitwae LUNA kuruka viunzi kama farasi.

MATOKEO KIDATO CHA SITA YAMETOKA.

Matokeo ya kidato cha 6 2011 yametoka,kwa habari zaidi bofya www.necta.go.tz/2011/alevel.htm

MACHAFUKO BAADA YA UCHAGUZI HUKO NIGERIA

Kumetokea machafuko ya kisiasa huko kaskazini mwa Nigeria baada ya kutangwaza matokeo ya uchaguzi uliofanyika Jumamosi, matokeo hayo yameonyesha Bw Goodluck Jonathan amemshinda mpinzani wake Bw Muhammadu Buhari. Vurugu hizo zimepeleka vifo vya watu sita na wengine kukimbia makazi yao. Taarifa zaidi zinaonyesha uwepo wa vifo vingi na hali kuwa mbaya zaidi.Machafuko yameshika kasi sana katika miji ya Kaduna na Kano.
Wananchi wakifanya vurugu huko Nigeria kaskazini

                                                                                       from aljazeera

NJIA ZA WAENDESHA BAISKELI

Huko London wenzetu wamepiga hatua kwa kuandaa njia maalum kwa waendesha baiskeli,njia hizo zimepakwa rangi ya blue.Njia hizo zimeanza kuwekwa huko West London,mikakati yao kufikia 2015 mji wote utakuwa na njia hizo.

KIBOKO WA RANGI YA PINKI

                             Umeiona hii??kiboko huyu anapatatikana Kenya.

HATIMAYE GBAGBO AKAMATWA.

Baada ya kung'ang'ania madaraka kwa muda mrefu,rais wa Ivory Coast Laurent Gbagbo amekamatwa na jeshi la nchi hiyo kwa ushirikiano wa jeshi la umoja wa mataifa Ufaransa.Wakilishi wa Ivory Coast katika Umoja wa Mataifa amesema  Gbagbo atafikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Rais Gbagbo akitolewa nje ya hoteli alipokuwa amejificha

Mwanajeshi akishangilia ushindi wa kumkamata Gbagbo
                           Mke wa Gbagbo,Bi Simone nae awekwa chini ya ulinzi

THE GAME NDANI YA KIJOGOO

Msanii The Game nae ameamua kutupia style ya Kijogoo a.k.a  KIDUKU kwenye kichwa chake.Style hii hapa nchini inapendwa sana na wasanii kutoka THT

VIKOMBE VYAZIDI KUTOLEWA!!!

Baada ya Mchungaji mstaafu Bw Ambilikile Masapile"BABU" kuja na dawa inayotibu magonjwa sugu "KIKOMBE" kaoteshwa na MUNGU.Sasa kumeibuka watu wengine wanaogawa dawa kwa mtindo huo wa KIKOMBE nao wanadai wameoteshwa!!

Babu akifanya vitu vyake.
Mfano huko Tabora amejitokea mwanamke anaetambulika kwa jina la Magret Mutalemwa a.k.a BIBI nae anagawa kikombe kwa madai kuwa ameoteshwa na Bikira Maria,tofauti na BABU,BIBI anatumia kikombe cha udongo huku akikushika kichwa wakati anakupa kikombe.Wagonjwa mbalimbali wametoa shuhuda za kupata nafuu baada ya kupata kikombe cha Bibi,huku wakiitaka serikali kupitia halmashauri ya Tabora kumsaidia BIBI kutoa huduma hiyo kwani mazingira ya kufika kwake sio mazuri.
                              bibi na kikombe chake.

Halikadhalika huko Pwani maeneo ya Ruvu Darajani amejitokeza kijana Juni Abunda aliyepewa jina la KAKA,nae anagawa kikombe kinachotibu magonjwa sugu kwa madai ya kuoteshwa na Mungu.Kaka yeye anatoa kikombe bure!!!
Wakati huohuo ahuko Mbeya Mchungaji Mwasumale wa kanisa la kinabii lililopo Tukuyu Rungwe nae anatoa kikombe.Mbali na hao Morogoro nako amejitokeza mwanamke mwingine anayeitwa Fatma Senga nae anagawa kikombe.Sasa sijui huyu ataitwa nani?? labda Shangazi.