PICHA YA WATOA KIMAISHA!!

Kwa miaka 11, Rozonno na mkewe Mia McGhee walifanya kila walichokiweza ili waweze kuzaa mtoto angalau mmoja,hatimaye mwaka jana mwezi juni Mia alifanikiwa kupata mimba na kujifungua si mtoto mmoja bali watoto mapacha sita

Lakini mahitaji ya watoto hao wachanga yalikuwa makubwa kuliko uwezo wao. Kwa siku watoto hao walitumia jumla ya nepi 50 na chupa 30 za maziwa
Mia alimwambia mumewe waweke pozi na watoto wao na walipiga picha ambayo Mia aliiweka kwenye mtandao wa Facebook kwani maombi yao ya msaada kwa manispaa yalikataliwa.

Picha hiyo ilijipatia umaarufu duniani na haikuchukua muda ilimfikia bilionea Oprah Winfrey ambaye alivutiwa na picha hiyo na kuamua kumualika Rozonno na mkewe kwenye shoo yake pia Oprah aliizawadia familia hiyo dola 250,000 za kufanya manunuzi ya mahitaji yao yote wakati wowote wanapotaka kwenye mtandao wa supermarket kubwa Marekani ya Walmart.

Ingawa Rozonno na mkewe walishaoana miaka 11 iliyopita walipokuwa na umri wa miaka 18 na 19, Oprah aliwazadia zawadi ya kwenda fungate (honeymoon) kwenye mojawapo ya hoteli kubwa za mjini Las Vegas.

No comments: