Afrika ikatae kunyonywa na kugawanywa


Baraza Kuu la  Umoja wa Mataifa,  mwishoni mwa wiki limepitisha kwa kauli moja  Tamko la Kisiasa kuhusu Utatuzi wa  Migogoro  Barani Afrika kwa njia ya  Amani.
Tamko hilo  ambalo ndani yake  linaainsha  na kutambua mchango mkubwa wa   Muungano wa Nchi Huru za Afrika  (OAU) na sasa Muungano wa Afrika ( AU)  katika kuchagiza  na kusimamia  pamoja na mambo mengine, maendeleo ya nchi za Afrika na watu wake,  kupiga vita  umaskini, ujenzi wa utawala bora, demokrasia , haki za  binadamu na utatuzi wa migororo kwa njia za amani.

Kabla ya kupitishwa kwa Tamko hilo,  Baraza Kuu la Umoja wa  Mataifa,  kwa siku nzima ya Alhamisi na ijumaa asubuhi lilijikita katika  majadiliano  ya mada iliyohusu ‘utatuzi wa migogoro kwa njia ya amani barani afrika’, ikiwa pia ni sehemu na  Baraza hilo kuadhimisha miaka  50   tangu kuanzishwa kwa OAU na baadaye AU.

Miongozi wa viongozi wakuu walioshirikia majadilaino hayo, na ambayo yaliandaliwa na Bw. Vuk Jeremic,   Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon,   Rais wa  Equatoria Guinea Theodore Obiang Nguema Mbasogo, Rais Mstaafu wa Burundi Jean Pierre Buyoya  ambaye pia     Mwakilishi  maalum wa Muungano wa Afrika  huko Mali na Sahel,  wakiwamo pia mawaziri  kadhaa wa  Mambo ya Nchi za Nje.

Akiungana na wazungumzaji wengine katika mkutano huo, Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Tuvako Manongi, pamoja na kuainisha sababu na vyanzo vya migogoro Barani Afrika, alisema, Afrika lazima ifikie mahali ikatae kugawanywa.
“Bara la Afrika lina fursa  nyingi,  Afrika inapanda chati. Afrika lazima ikatae kugawanywa, ikatae kudharauliwa na ikatae  kunyonywa” akasema Mwakilishi wa Kudumu, Tuvako Manongi.

Na kubainisha kwamba,  Afrika lazima pia ikatae kutambuliwa kama bara ambalo limejaa migogoro  . “  Huu ni wakati wa  kufufua  upya pan africanism,  hiki ni kipindi cha mwamko mpya wa Afrika. Lazima tufanye kazi kwa pamoja  ili kuwapa matumaini watu wetu” akasisitiza Manongi.

Wakati tukisherehekea maadhimisho ya miaka 50 wa OAU,  ni  vema kila mmoja wetu akaahidi  upya  kuimarisha ushirikiano kati ya Umoja wa Mataifa na
Muungano wa Afrika  kama ilivyoainishwa  katika  Sura ya Saba ya Katima ya Umoja  wa Mataifa.

Akatoa mfano kwa kusema  uhusiano huo unapashwa kuendelezwa katika nyanja zote za  usalama na  maendeleo.  Kama ambavyo imeshashuhudiwa  katika   uundwaji wa Jeshi la  Mseto  kati ya Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika   katika Jimbo la Darfur ( UNAMID),  Misheni ya  Muungano wa Afrika huko Somalia, (AMISOM0  na tukio la hivi karibuni la kurejewa na  kuongozewa uwezo mpya Misheni ya Kutuliza Amani katika DRC ( MONUSCO) kulikoendana na kuridhiwa  upelekaji wa Brigedi Maalum inayoundwa na wanajeshi kutoka Tanzania, Afrika ya Kusini na Malawi.

Aidha akasema majadiliano hayo  ya Baraza  Kuu la Umoja wa Mataifa, yamefanyika ikiwa  ni siku chache tu,   tangu kufanyika kwa Mkutano wa Baraza la Usalama la Afrika katika ngazi ya Mawaziri nchini Tanzania,  mkutano ambao pia ulijadili kwa kina pamoja na mambo mengine  hali ya usalama  barani afrika , vyanzo vya migogoro na ufumbuzi wake.
Karibu wazungumzaji wote wakiwamo wawakilishi wa Marekani na Jumuiya ya Ulaya waliochangia majadialiano hayo ya utanzuaji wa migogoro kwa njia ya amani, licha ya  kutambua, kusifu na kupongeza kazi kubwa ambayo imefanywa na inaendelea kufanywa na   Muungano wa  Afrika na Taasisi za Kikanda katika kipindi cha miaka 50 iliyopita, walisisitiza haja na  umuhimu wa Jumuiya ya Kimataifa kuendeleza ushirikiano wake na Muungano wa Afrika.

Aidha wazungumzaji huo walitambua na kukiri kwamba  Bara la Afrika licha ya  changamoto mbalimbali zikiwamo za migogoro inayoibuka hapa na pale,  imepiga hatua kuubwa za kimaendeleo, kiuchumi na kijamii na kwamba   Bara hilo linastahili kupongezwa na kuendelea kusaidiwa.

Arudi shule baada ya utafiti wa TAMWA




UTAFITI wa kihabari uliofanywa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Machi 2012 umefanikisha kumrudisha shuleni mwanafunzi wa sekondari aliyekuwa ametelekezwa yeye pamoja na familia yao.

Mwenjuma Magalu ambaye kwa sasa ni mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari Komnyang'anyo alitelekezwa na babayake yeye pamoja na mamayake mwaka jana, hivyo kushindwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule hiyo licha ya kuchanguliwa kuendelea na masomo.

Hata hivyo baada ya utafiti wa kihabari kufanyika kijijini Msasa Wilaya ya Handeni na taarifa za mtoto huyo kushindwa kujiunga na sekondari baada ya mamayake (kwa sasa marehemu) kukosa uwezo kuripotiwa, alijitokeza mfadhili wa kumsomesha ambaye anagharamia masomo yake hadi sasa.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi juzi akiwa shuleni Komnyang'anyo, mwanafunzi huyo aliishukuru TAMWA kwa kuibua tatizo la familia yao kwa umma na kupatikana kwa mfadhili ambaye amemrudisha masomoni licha ya familia yao kutelekezwa.

"Binafsi nawashukuru sana hao (TAMWA) waliopaza sauti hadi mjuu wangu kurudi shuleni...hii kwetu ilikuwa ni ndoto kwetu maana mtoto mwenyewe alikuwa amekata tamaa kabisa kurudi shuleni na alikuwa kaanza kufanya vibarua mitaani huku wenzake wakiendelea na shule," alisema bibi wa mtoto huyo, Amina Mohamed akizungumza.

Bibi huyo akizungumzia maisha ya sasa ya familia hiyo alisema bado wanahitaji msaada wa huduma hasa baada ya mwanaye kufariki dunia mwaka jana na kumuachia watoto wake.

Aliongeza kwa sasa yeye ni mgonjwa wa TB anayetumia dawa hivyo kwa hali yake ameshauriwa kupumzika jambo ambalo limempa mzigo mkubwa kimajukumu mwanafunzi (Mwenjuma), kufanya kazi za nymbani kama kupika kulima na shughuli nyingine.


Hata hivyo mama wa mtoto huyo (Hadija Magalu) ambaye alitelekezwa na mzazi mwenzake alifariki dunia mwaka jana kwa tatizo la uzazi na kuiacha tena familia hiyo ya watoto watatu katika hali ngumu zaidi chini ya malezi ya bibi mzaa mama.

kwa hisani ya mjengwablog

24 Kilwa villagers set up 60-ha sesame demonstration farm # keep it up AMSHA

Twenty four farmers at Tilawandu village, Kilwa district in Lindi region have introduced a demonstration farm for sesame production for other villagers from the district to learn from.

Institutional Coordinator of the Amsha Institute of Rural Entrepreneurs East Africa, Omari Mwaimu told The Guardian on Saturday that villagers have decided to establish the demonstration farm to help farmers shift from traditional farming system to commercial farming.

The farm will enable more than 300 farmer groups in the district to learn from it to boost their economic fortunes , improve farmer’s network and facilitate the development of sesame production within the country.

“As I speak to you now some 150 acres of land has been cultivated and allocated as demonstration farms at Tilawandu village,” he said.

He said commercial farming is way that farmer plant various crops and harvest it for sell to get profit.

This is a new strategy designed by farmers so that they can access reliable market for their produce, assist them increase their incomes and improve their livelihoods.

According to Mwaimu, once they farmers acquire some knowledge on sesame production Amsha Institute in collaboration with Naliendele Agricultural Research Institute will provide seeds to farmers, loans to purchase pesticides, provide technical training on soil conservation, controlling pests and diseases and post-harvest storage including improvement of the quality of their produce through training on storage,” he said.

They will train farmers on accessing up to date market prices information and negotiation skills so that they can obtain a fair price for their produce from buyers or brokers to benefit from what they grow.
The groups will also be linked to markets so that they coul access reliable market for their crop.

“There is a need to educate them on commercial farming because sesame has a lot of health benefits because it is among the seeds rich in quality vitamins and minerals.

They are very good sources of B-complex vitamins such as niacin, folic acid, thiamin (vitamin B1), pyridoxine (vitamin B6), and riboflavin,” he said.

“I believeimproved seeds and farming techniques would be introduced to many farmers and that the majority of farmers will benefit from what they grow and shift from traditional farming system,” he noted.

Elaborating on how small holders in Kilwa district are being supported, he said as Amsha Institute normally use member’s fees to sensitize farmers to change their mindset and convert their traditional farming system to commercial agriculture.

According to officials although Tanzania is the world’s 12th largest sesame producer, still farmers in other areas cannot meet existing demand as they lack access to seed varieties, capacity building and even technologies that would improve production within their respective farms.

To meet this demand Amsha Institute is working with Naliendele Agricultural Research Institute and Tanzania Graduate Farmers Association (TGFA) to train farmers on commercial farming to assist farmers increase sesame production and link them to markets which will significantly improve their income and livelihoods, enabling them to purchase additional food, household goods and pay for school costs.

The seeds are an also very valuable source of dietary proteins with fine quality amino acids that are essential for growth, especially in children. Just 100g of seeds provide about 18 g of protein (32 percent of daily-recommended values), according to experts.

Atoka Mbeya mpaka Dar es Salaam kwa baiskeli

Katika hali ambayo humkuta kila mwanadamu kutaka kutumia kipaji chake ili kujipatia kipato binafsi, kijana John Mwaipaya kutoka Songwe jiji Mbeya amechukua maaumuzi ya kuja jiji Dar es Salaam kuendeleza michezo yake ya baiskeli. Anasema kilichomfanya aje jijini Dar, baada ya kutopata mafanikio jiji Mbeya kupitia mchezo huo, hivyo amekuja Dar kutafuta wafadhili watakao msaidia kukuza na kuendeleza kipaji chake cha michezo ya baiskeli. "Mbeya kazi ilikua ngumu sana, yaani nimejitahidi kutunga michezo mingi na kuionyesha lakini hakuna mtu anayeithamini,hivyo nilisikia Dar kuna watu wanaoweza kunisaidia kuendeleza michezo yangu" amesema John.

Michezo hii,nimeigundua mwenye,hakuna aliyenifundisha na nimeifanya kwa muda wa miaka nane sasa aliongeza bwana John.
Anasema alipofika Dar amekuta mambo ni tofauti na alivyofikiri kwani imekua ni ngumu kupata mtu wa kuendeleza kipaji hicho. Nilipofika Dar, nilifikia Ukonga kwa shemeji yangu, lakini kwa niliondoka baada ya muda mfupi kutoka ungumu pale nyumbani kwa sasa  nipo Magomeni amesema bwana John.
Halidhalika bwana John amesema anafanya shughuli hiyo kwa kuzunguka sehemu mbalimbali na kuonyesha michezo hiyo."Huwa watu wanajikusanya kila mwenye kiasi chochote hutoa halafu ndo naanza kuonyesha" amesema bwana John. Ninachokipata ni kiasi kinachoniwezesha kupata hela ya kula tu.

Bwana John ana ndoto za kufungua chuo kitakachowafundisha vijana michezo mbalimbali ya baiskeli. Hivyo kufanya fani hiyo kuwa sehemu itakayowawezesha vijana kujipatia ajira rasmi.


HAPA NA PALE SJMC WIKI HII

Kushoto ni Sam Sebastian akiwa na Jeff Kijanga  kabla ya kuingia pindi

Tulipoingia sasa akaanza kupiga Injili kukemea pepo

Bi dada Josephine nae akajiachia kamera

Kevoo unajificha au ndo unatoa tano??

You may call him King Vesso himself akitokelezea ki-corporate zaidi.

Busy kwenye kimbweta, kwa mbali ni Mudi Said
Michakato ikiwekwa sawa

Asante sana, Aggie a.k.a Mama Alvin. U show us what got.

Sweet dadaz, Teddy and Maggie
Mzee wa Dhofulihali, Cholo boy akiwa ndani ya IT
Hawa ni baadhi tu ya walioweza kujiachia na kamera kwa wiki hii. Kama hukubahatika may next time.

Picha kwa hisani ya Nyayo Studios