Kinabo mhitimu SUA aliejiajiri katika ufugaji wa samaki
Mawazo ya wahitimu wengi wa vyuo vikuu
nchini katika miaka ya karibuni imekuwa ni namna ya kupata ajira
zenye tija.
Hata
hivyo, baadhi wamekumbana na tatizo la ajira ambalo limewasukuma katika kubuni
miradi ambayo itawawezesha kumudu maisha na changamoto zake.
Mmoja wao, Simon Kinabo, mhitimu wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kilichoko Morogoro ameamua kujiajiri baada ya kubuni mradi wa ufugaji wa samaki.
Ndoto
ya wengi ni kupata kazi za kipato kizuri na ambazo zitawawezesha kuishi vizuri,
kumiliki gari, kujenga nyumba na mambo mengine lukuki.
Hata
hivyo, baadhi wamekumbana na tatizo la ajira ambalo limewasukuma katika kubuni
miradi ambayo itawawezesha kumudu maisha na changamoto zake.Mmoja wao, Simon Kinabo, mhitimu wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kilichoko Morogoro ameamua kujiajiri baada ya kubuni mradi wa ufugaji wa samaki.
Mradi
huo unaoitwa Rombo Unique Aquaculture, upo kilomita 60 kutoka mjini Moshi
na kilomita nne kutoka makao makuu ya Wilaya ya Rombo, eneo la Mkuu.
Anasema akiwa mwanafunzi katika chuo hicho, akisomea Shahada ya Sayansi ya Viumbe wa Majini (BSc Aquaculture) alihamasika na somo la uzalishaji wa samaki na ndipo akaamua kuanzisha mradi huo kwa mtaji wake.
Anasema akiwa mwanafunzi katika chuo hicho, akisomea Shahada ya Sayansi ya Viumbe wa Majini (BSc Aquaculture) alihamasika na somo la uzalishaji wa samaki na ndipo akaamua kuanzisha mradi huo kwa mtaji wake.
“Katika
fedha zile za mkopo, kila nikipewa na Serikali, nilichukua kiasi kidogo
na kuanzisha nyumbani mradi wa kufuga samaki.
Niliamini ni mradi mzuri ambao unaweza kubadili maisha yangu,” anasema.
Anaongeza kuwa alianzisha mradi huo kwa kuchimba bwawa dogo na kuanza kuzalisha samaki, kwa lengo la kuja kuwauza baadaye.
Niliamini ni mradi mzuri ambao unaweza kubadili maisha yangu,” anasema.
Anaongeza kuwa alianzisha mradi huo kwa kuchimba bwawa dogo na kuanza kuzalisha samaki, kwa lengo la kuja kuwauza baadaye.
Mkopo
wa CRDB
Anasema akiwa mwaka wa pili SUA alipata taarifa ya kuwapo mradi wa SUGECO unaoendeshwa na chuo hicho na CRDB ambao unalenga kuwawezesha wanafunzi wa elimu ya juu kuingia katika ujasiriamali.
Anasema akiwa mwaka wa pili SUA alipata taarifa ya kuwapo mradi wa SUGECO unaoendeshwa na chuo hicho na CRDB ambao unalenga kuwawezesha wanafunzi wa elimu ya juu kuingia katika ujasiriamali.
“Baada
ya kupata taarifa hizo nilijitokeza kuandika andiko la kuomba fedha na baada ya
usaili, andiko langu lilipitishwa na chuo na CRDB,” anasema.
Anaongeza kuwa baada ya kupitishwa andiko lake, alipokea mkopo wa Sh20 milioni kwa ajili ya kuanzisha mradi.
Anaongeza kuwa baada ya kupitishwa andiko lake, alipokea mkopo wa Sh20 milioni kwa ajili ya kuanzisha mradi.
Baada
ya kupokea fedha, aliamua kupanua bwawa hilo na pia kuliongezea mifumo ya
kuingiza maji kutoka Mto Ngwasi na kutoamaji ili liwe la kisasa.
“Nilinunua mabomba 100 ya futi 2,000 na sasa bwawa langu lina urefu chini, mita tatu hadi sita na upana mita 30,” anaeleza.
“Nilinunua mabomba 100 ya futi 2,000 na sasa bwawa langu lina urefu chini, mita tatu hadi sita na upana mita 30,” anaeleza.
Anasema
kuwa baada ya upanuzi wa bwawa alinunua samaki wadogo 3,000 kutoka Gereza la
Karanga mjini Moshi ambao walikuwa ni wa jamii ya perege na kambare.
Anaongeza kuwa kila kifaranga cha samaki alikinunua kwa Sh300 na kwamba hiyo ilikuwa Mei 5, mwaka jana, alipoanza kuwapandikiza bwawani mwake.
Anaongeza kuwa kila kifaranga cha samaki alikinunua kwa Sh300 na kwamba hiyo ilikuwa Mei 5, mwaka jana, alipoanza kuwapandikiza bwawani mwake.
Mafanikio
ya mradi
Hadi sasa, Kinabo anasema bwawa lake linao zaidi ya samaki 40,000, kati ya hao wakubwa ni 10,000 na wadogo 30,000.
Anasema , Juni mwaka huu anatarajia kuanza kuvua samaki na matarajio yake ni kuvua tani nne za samaki.
“Nina imani tani hizo nne, nikivua naweza kupata zaidi ya Sh60 milioni na tayari nimepata masoko,” anasema msomi huyo.
Hadi sasa, Kinabo anasema bwawa lake linao zaidi ya samaki 40,000, kati ya hao wakubwa ni 10,000 na wadogo 30,000.
Anasema , Juni mwaka huu anatarajia kuanza kuvua samaki na matarajio yake ni kuvua tani nne za samaki.
“Nina imani tani hizo nne, nikivua naweza kupata zaidi ya Sh60 milioni na tayari nimepata masoko,” anasema msomi huyo.
Anasema
tayari, amefanya mazungumzo na wakuu wa shule kadhaa za sekondari
wilayani Rombo, Hospitali ya wilaya hiyo na maeneo kadhaa ambao wamekubali
kununua samaki wake.
Kwa
kutambua kuwa hawezi kufanya kazi hizo peke yake, mjasiriamali huyo msomi
amemwajiri mtunza mazingira, James Edmund, pia hivi karibuni atakuwa na
walinzi wawili na muuzaji wa samaki.
kwa hisani yamwanachi
Afrika ikatae kunyonywa na kugawanywa
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, mwishoni mwa wiki limepitisha kwa kauli moja Tamko la Kisiasa kuhusu Utatuzi wa Migogoro Barani Afrika kwa njia ya Amani.
Tamko hilo ambalo ndani yake
linaainsha na kutambua mchango mkubwa wa Muungano wa Nchi
Huru za Afrika (OAU) na sasa Muungano wa Afrika ( AU) katika
kuchagiza na kusimamia pamoja na mambo mengine, maendeleo ya nchi
za Afrika na watu wake, kupiga vita umaskini, ujenzi wa utawala
bora, demokrasia , haki za binadamu na utatuzi wa migororo kwa njia za
amani.
Kabla ya kupitishwa kwa Tamko hilo,
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, kwa siku nzima ya Alhamisi na
ijumaa asubuhi lilijikita katika majadiliano ya mada iliyohusu
‘utatuzi wa migogoro kwa njia ya amani barani afrika’, ikiwa pia ni sehemu
na Baraza hilo kuadhimisha miaka 50 tangu kuanzishwa
kwa OAU na baadaye AU.
Miongozi wa viongozi wakuu walioshirikia
majadilaino hayo, na ambayo yaliandaliwa na Bw. Vuk Jeremic, Rais
wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki
Moon, Rais wa Equatoria Guinea Theodore Obiang Nguema
Mbasogo, Rais Mstaafu wa Burundi Jean Pierre Buyoya ambaye
pia Mwakilishi maalum wa Muungano wa Afrika
huko Mali na Sahel, wakiwamo pia mawaziri kadhaa wa Mambo ya
Nchi za Nje.
Akiungana na wazungumzaji wengine katika
mkutano huo, Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Tuvako
Manongi, pamoja na kuainisha sababu na vyanzo vya migogoro Barani Afrika,
alisema, Afrika lazima ifikie mahali ikatae kugawanywa.
“Bara la Afrika lina fursa
nyingi, Afrika inapanda chati. Afrika lazima ikatae kugawanywa, ikatae
kudharauliwa na ikatae kunyonywa” akasema Mwakilishi wa Kudumu, Tuvako
Manongi.
Na kubainisha kwamba, Afrika lazima
pia ikatae kutambuliwa kama bara ambalo limejaa migogoro . “ Huu ni
wakati wa kufufua upya pan africanism, hiki ni kipindi
cha mwamko mpya wa Afrika. Lazima tufanye kazi kwa pamoja ili kuwapa
matumaini watu wetu” akasisitiza Manongi.
Wakati tukisherehekea maadhimisho ya
miaka 50 wa OAU, ni vema kila mmoja wetu akaahidi upya
kuimarisha ushirikiano kati ya Umoja wa Mataifa na
Muungano wa Afrika kama
ilivyoainishwa katika Sura ya Saba ya Katima ya Umoja wa
Mataifa.
Akatoa mfano kwa kusema uhusiano
huo unapashwa kuendelezwa katika nyanja zote za usalama na
maendeleo. Kama ambavyo imeshashuhudiwa katika
uundwaji wa Jeshi la Mseto kati ya Umoja wa Mataifa na Muungano wa
Afrika katika Jimbo la Darfur ( UNAMID), Misheni ya
Muungano wa Afrika huko Somalia, (AMISOM0 na tukio la hivi karibuni la
kurejewa na kuongozewa uwezo mpya Misheni ya Kutuliza Amani katika DRC (
MONUSCO) kulikoendana na kuridhiwa upelekaji wa Brigedi Maalum inayoundwa
na wanajeshi kutoka Tanzania, Afrika ya Kusini na Malawi.
Aidha akasema majadiliano hayo ya
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, yamefanyika ikiwa ni siku chache
tu, tangu kufanyika kwa Mkutano wa Baraza la Usalama la Afrika
katika ngazi ya Mawaziri nchini Tanzania, mkutano ambao pia ulijadili kwa
kina pamoja na mambo mengine hali ya usalama barani afrika , vyanzo
vya migogoro na ufumbuzi wake.
Karibu wazungumzaji wote wakiwamo wawakilishi
wa Marekani na Jumuiya ya Ulaya waliochangia majadialiano hayo ya utanzuaji wa
migogoro kwa njia ya amani, licha ya kutambua, kusifu na kupongeza kazi
kubwa ambayo imefanywa na inaendelea kufanywa na Muungano wa
Afrika na Taasisi za Kikanda katika kipindi cha miaka 50 iliyopita,
walisisitiza haja na umuhimu wa Jumuiya ya Kimataifa kuendeleza
ushirikiano wake na Muungano wa Afrika.
Aidha wazungumzaji huo walitambua na
kukiri kwamba Bara la Afrika licha ya changamoto mbalimbali
zikiwamo za migogoro inayoibuka hapa na pale, imepiga hatua kuubwa za
kimaendeleo, kiuchumi na kijamii na kwamba Bara hilo linastahili
kupongezwa na kuendelea kusaidiwa.
Arudi shule baada ya utafiti wa TAMWA
UTAFITI wa kihabari uliofanywa
na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Machi 2012
umefanikisha kumrudisha shuleni mwanafunzi wa sekondari aliyekuwa ametelekezwa
yeye pamoja na familia yao.
Mwenjuma Magalu ambaye kwa sasa
ni mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari Komnyang'anyo
alitelekezwa na babayake yeye pamoja na mamayake mwaka jana, hivyo kushindwa
kujiunga na kidato cha kwanza katika shule hiyo licha ya kuchanguliwa kuendelea
na masomo.
Hata hivyo baada ya utafiti wa
kihabari kufanyika kijijini Msasa Wilaya ya Handeni na taarifa za mtoto huyo
kushindwa kujiunga na sekondari baada ya mamayake (kwa sasa marehemu) kukosa
uwezo kuripotiwa, alijitokeza mfadhili wa kumsomesha ambaye anagharamia masomo
yake hadi sasa.
Akizungumza na mwandishi wa
habari hizi juzi akiwa shuleni Komnyang'anyo, mwanafunzi huyo aliishukuru TAMWA
kwa kuibua tatizo la familia yao kwa umma na kupatikana kwa mfadhili ambaye
amemrudisha masomoni licha ya familia yao kutelekezwa.
"Binafsi nawashukuru sana
hao (TAMWA) waliopaza sauti hadi mjuu wangu kurudi shuleni...hii kwetu ilikuwa
ni ndoto kwetu maana mtoto mwenyewe alikuwa amekata tamaa kabisa kurudi shuleni
na alikuwa kaanza kufanya vibarua mitaani huku wenzake wakiendelea na
shule," alisema bibi wa mtoto huyo, Amina Mohamed akizungumza.
Bibi huyo akizungumzia maisha
ya sasa ya familia hiyo alisema bado wanahitaji msaada wa huduma hasa baada ya
mwanaye kufariki dunia mwaka jana na kumuachia watoto wake.
Aliongeza kwa sasa yeye ni
mgonjwa wa TB anayetumia dawa hivyo kwa hali yake ameshauriwa kupumzika jambo
ambalo limempa mzigo mkubwa kimajukumu mwanafunzi (Mwenjuma), kufanya kazi za
nymbani kama kupika kulima na shughuli nyingine.
Hata hivyo mama wa mtoto huyo
(Hadija Magalu) ambaye alitelekezwa na mzazi mwenzake alifariki dunia mwaka
jana kwa tatizo la uzazi na kuiacha tena familia hiyo ya watoto watatu katika
hali ngumu zaidi chini ya malezi ya bibi mzaa mama.
kwa hisani ya mjengwablog
Subscribe to:
Posts (Atom)
